Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, February 4, 2013

CCM MKOA KILIMANJARO YAADHIMISHA MIAKA 36 HAPO JANA TANGU KUZALIWA KWA CHAMA HICHO

 

Jana katika viwanja vya kata ya Pasua iliyo ndani ya Manispaa ya Moshi, Kulirindima shamrashamra ya sherehe za maadhimisho ya miaka 36 ya kuzaliwa kwa Chama hicho. Akipokea Maandamano makubwa ya wanachama wa CCM yaliyokuwa yakiongozwa na Kamanda wa Vijana na Mjumbe wa NEC moshi mjini Ndugu Agrey Mareale, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mh. LEonidas Gama alisema Furaha ya Maadhimisho haya iambatane na Utekelezaji wa Sera ya chama cha mapinduzi ya kulinda amani na kuchochea Maendeleo na yeye kama Mwakilishi wa Serikali ya CCM ndani ya Mkoa wa Kilimanjaro atahakikisha anasimamia hilo.

 

Katibu wa CCM mkoa kilimanjaro Mh Kazidi, Akimtambulisha Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Kilimanjaro Mh. Idi Juma



Hata hivyo Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro ndugu Kazidi aliongeza kwa kusema CCM hawatojibu matusi yanayotolewa na CHADEMA dhidi yao na akamuomba mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro kutojibu matusi anayotukanwa kila mara katika mikutano yao kwa sababu tu anasimamia vyema fedha za wananchi wa moshi zisitumiwe kinyume na Taratibu.

 

Mwenyekiti wa CCM mkoa kilimanjaro akipokea kadi za wanachama wapya wanaotoka vyama vya upinzani hapo jana

 

 

Katibu huyo ameweza kuelezea mambo mbalimbali yaliyofanywa na serikali ya ccm katika mkoa wa Kilimanjaro kama kujenga barabara, kukarabati barabara, kujenga shule za kata, Zahanati na hata kuwezesha kuwapa elimu ya ujasiria mali vikundi mbalimbali ili kuweza kujiajiri ambapo moja ya utekelezaji wa ilani ya ccm ni Sacoss mbambali zilizofunguliwa.

Pia waliweza kupokea vikundi mbali vya vijana na wakina mama waliweza kurudisha kadi za Upinzani na kuahidi kufanya kazi ya kutoa elimu dhidi ya uzalendo kwa wananchi wanaotangaziwa siasa za uvunjaji wa amani.

No comments:

Post a Comment