Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, March 1, 2013

MOSHI KWACHAFUKAAAAAAAAAAAAA!!!



Ikiwa ni siku moja tu imebakia kufika siku ya jumapili, Siku ya Mbio za Kilimanjaro Marathon zinazofanyika kila mwaka nchini Tanzania Mkoani Kilimanjaro. Moshi kumefurika watu.

Wakati unaingia ndani ya Mji wa Moshi utakutana na mabango makubwa pembezoni mwa barabara yanayokuashiria kuwa kuna tukio kubwa limewadia mjini Moshi, Si lingine ni Kilimanjaro Marathon 2013.

                               Hili ndilo Bango linalokukaribisha ndani ya Mji wa Moshi

Hali ya kiburudani imeanza toka wiki iliyopita mji wa Moshi a na umechangamshwa na leo katikati ya viunga vya mji wa Moshi katika barabarA ya Voda Club linadondoka bonge la Event litakalohusisha wapenzi wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager na wakimbiaji wa mbio za Kilimanjaro marathon maarufu kama Kili Marathon iliyodhaminiwa na Kampuni ya bia Tanzania. {TBL} ku kupitia Bia ya Kilimanjaro Premium Lager.


 Anaitwa Abraham ni Sound Engineer wa Bills akihakikisha  sound inakaa vizuri leo

Leo anzia saa moja jioni kutakua na burudani kibao kutoka kwa Twanga Pepeta, Joh makini, Warior band from the east na wengine kibao huku nyama choma na bia vikiwa vimesambaa kila kona.
Kama huna pesa bora ulale……! Mimi nitakuwepo.


                                      Stage ikiwa imesimama vyema nje ya voda Shop

No comments:

Post a Comment