MKAZI mmoja wa Kitasha Mengeni wilayani Rombo aliyefahamika kwa jina la Balthazar Pankras Swai mwenye umri wa miaka 49 anashikiliwa na Jeshi
la Polisi kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi wa darasa la tano
mwenye ulemavu wa akili. Na taarifa kutoka katika jeshi la polisi zinadhibitisha kutokea kwa tukio hilo usiku wa kuamkia tarehe 25 Aprili 2013 katika kijiji cha Aleni Chini.
Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro limesema kitendo hicho cha kikatili alichofanyiwa mwanafunzi huyo wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Mengeni wilayani Rombo, kimemsababishia mtoto huyo maumivi makali katika sehemu zake siri. Mbinu iliyotumika kumkamata mzee huyo ni polisi wakishirikiana na polisi jamii wa kijiji hicho kwa usimamizi wa Mwenyekiti Correntini Masawe.
Jeshi la Polisi mkoani Kilimanjaro limesema kitendo hicho cha kikatili alichofanyiwa mwanafunzi huyo wa darasa la tano katika Shule ya Msingi Mengeni wilayani Rombo, kimemsababishia mtoto huyo maumivi makali katika sehemu zake siri. Mbinu iliyotumika kumkamata mzee huyo ni polisi wakishirikiana na polisi jamii wa kijiji hicho kwa usimamizi wa Mwenyekiti Correntini Masawe.
Mashuhuda wa tukio hilo wamesema mtuhumiwa pia ni mhalifu sugu kwani alishawahi kufungwa gerezani miaka ya nyuma kutokana na matukio ya kihalifu huku wakilaani kitendo alichokifanya mtuhumiwa na kuvitaka vyombo vya dola kuchukua mkondo wake.
No comments:
Post a Comment