Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dk. Jakaya
Mrisho Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya ulinzi na usalama
lililoandaliwa maalum kwa ajili maadhimisho ya miaka 49 ya Muungano wa
Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika kwenye uwanja wa Uhuru leo jijini
Dar es salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, Vyama
vya Siasa na Mabalozi pamoja na wageni waalikwa mbalimbali ili
kushuhudia maadhimisho hayo.(PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-UWANJA
WA UHURU)
Rais Wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein kulia akiwa na viongozi wengine
katika jukwaa kuu kutoka kushoto ni Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi,
Makamu wa pili wa Rais Zanzibar Balozi Seif Idd, Mke wa Rais Mama Salma
Kikwete na Waziri Mkuu Mizengo Pinda.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Jakaya
Kikwete akiingia uwanjani katika gari maalum huku akisindikizwa na Mkuu
wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange.
Vikosi vilivyo pita na kutoa heshima mbele, kikosi cha Ulinzi JWTZ,
kikosi cha Jeshi la Ulinzi JWTZ, Kikosi cha Jeshi la Kujenga taifa JKT
na Kikosi Maalum Cha Bendera kikitoa heshima zake bele ya Rais Jakaya
Kikwete.
Watoto wa halaiki wakionyesha ujumbe mbalimbali kuhusu Muungano wetu
mbele ya Rais Jakaya Kikwete na maelfu ya Watanzania waliohudhuria
katika maadhimisho hayo.
Chanzo: fullshangweblog.com
No comments:
Post a Comment