Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, June 12, 2013

POLISI WANUFAIKA NA USHIRIKIANO WA POLISI WA BAVARIA,UJERUMANI ..!


Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Jimbo la Bavaria na Rais wa Chuo cha Polisi Bavaria cha Nchini Ujerumani Bw. Wolfgang Sommer  akiongea na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema wakati wakiwa katika kikao cha pamoja na maafisa wa Polisi Makao Makuu.Bw.Sommer yupo katika ziara ya kutembelea na kujionea mafanikio ya Jeshi la Polisi Tanzania (Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)


Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Jimbo la Bavaria na Rais wa Chuo cha Polisi Bavaria cha Nchini Ujerumani Bw. Wolfgang Sommer  akimkabidhi zawadi  Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Said Mwema wakati  wa ziara ya kutembelea na kujionea mafanikio ya Jeshi la Polisi Tanzania (Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)



Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Jimbo la Bavaria na Rais wa Chuo cha Polisi Bavaria cha Nchini Ujerumani Bw. Wolfgang Sommer  akiangalia jinsi ya uendeshaji wa mafunzo katika Gym ya Polisi iliyopo katika Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam (DPA) wakati wa ziara ya kutembelea na kujionea mafanikio ya Jeshi la Polisi Tanzania (Picha na Frank Geofray-Jeshi la Polisi)
…………………………………………………………..
Na Frank Geofray-Jeshi la Polisi
Jeshi la Polisi nchini limefaidika kwa kiasi kikubwa na ushirikiano uliopo kati yake na  chuo cha Bavaria cha Ujerumani  katika Nyanja za mafunzo, vifaa na polisi jamii jambo ambalo limewezesha maboresho ya jeshi hilo kuendelea vyema na kutoa huduma inayostahili kwa wananchi.
Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Jimbo la Bavaria na Rais wa Chuo cha Bavaria cha Nchini Ujerumani Wolfgang Sommer alipotembelea Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na baadhi ya  vikosi vya Jeshi hilo kujionea mafanikio ya Polisi jamii pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo katika utendaji wao wa kuimarisha usalama wa raia na mali zao hapa nchini.
Akizungumza katika ziara hiyo Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Paul Chagonja alisema ushirikiano baina ya chuo hicho na polisi umesaidia kwa kiasi kikubwa katika kupata mafunzo ya jinsi ya kuimarisha mkakati wa polisi jamii pamoja na jinsi ya kuboresha mitaala katika vyuo vyetu vya polisi.
“Ujerumani ni moja ya nchi zilizoendelea sana duniani hivyo na sisi kupitia maboresho yetu tuna mambo mengi ya kujifunza ili kuendana na usasa unaohitajika katika kuwahudumia wananchi wa Tanzania katika nyanja ya usalama”Alisema Kamishna Chagonja.
Kwa upande wake Mkuu wa Polisi jimbo la Bavaria na Rais wa Chuo cha Bavaria cha Ujerumani Wolfgang Sommer alisema majeshi ya Polisi hivi sasa duniani yanakabiliwa na changamoto nyingi kutokana na kuibuka kwa wahalifu wenye kutumia mbinu zilizoendelea hivyo Polisi wana wajibu wa kujifunza kwa kasi mbinu hizo.
Bw.Sommer alisema Polisi kote duniani wapo katika maboresho hivyo kwa siku zijazo majeshi hayo yataimarika katika kupambana na uhalifu na lengo la ziara yake ni kujifunza mbinu zinazotumiwa na polisi wa Tanzania katuika kukabiliana na uhalifu.

Katika ziara hiyo alitembelea Kikosi cha matengenezo ya magari ya Polisi ambacho kwa kiasi kikubwa kilifadhiliwa na Serikali ya Ujerumani mwaka 1994, Kikosi cha Mbwa na farasi, Chuo cha Taaluma ya Polisi (DPA), Kikosi cha Polisi Anga pamoja na vikundi vya ulinzi shirikishi vilivyopo katika Kanda Maalumu ya Dar es Salaam.
YOU MIGHT ALSO LIKE THIS

No comments:

Post a Comment