HABARI zilizotufikia hivi Punde zinasema
kwamba mwanafunzi ALEX ROBERT wa chuo kikuu DAR ES SALAAM (UDSM)
amefariki dunia mchana huu katika HOSPITALI YA TAIFA YA MUHIMBILI ambapo
alikuwa amelazwa kutokanana kujeruhiwa na risasi ambyo alipigwa na
majambazi walimvamia akiwemo yeye pamoja na wenzake watatu.
Taarifa
zilizotufikia katika chumba cha habari zinaeleza kuwa wanafunzi wanne
wa chuo kikuu cha Dar es salaam maarufu kwa jina la Chuo cha Mlimani
walivamiwa na majambazi usiku wa kuamkia jana maeneo ya Yombo chuoni
hapo.
Wanafunzi hao wanaosemekana kuwa ni wa mwaka wa nne na wa
mwisho wa masomo walikuwa wanajisomea na kuandaa “Disertation” zao na
kujikuta wakivamiwa na watu wanne na kuamuriwa watoe komputa zao na
pochi za fedha. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kutoka chuoni hapo,
wanafunzi hao walikubali kuwapa komputa hizo na pochi za fedha, na
majambazi kuanza safari yao.

Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala (Soft Copy) ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.
MUNGU AILAZE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA KIJANA ALEX ROBERT.. AMINA


Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala (Soft Copy) ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.

No comments:
Post a Comment