Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, July 8, 2013

Raisi Mstaafu wa Tanzania Ali Hassan Mwinyi akamilisha Tamasha la kiswahili pamoja na sherehe ya Miaka 3 ya Vijimambo.!

Rais Mustaafu Ali Hassan Mwinyi Siku ya Jumamosi July 6, 2013  katika ukumbi wa Hamton Place ameweza kukamilisha sherehe za miaka 3 ya blog ya Vijimambo pamoja na Tamasha la Kishwahili lililoandaliwa na Jumuiya ya waTanzania pamoja na uongozi mzima wa Ubalozi wa Tanzania Jijini Washington DC 
Rais Mustaafu Ali Hassan Mwinyi akiwa na mkewe wakiangalia bidhaa mbali mbali ziliwakilishwa na wajasiri mali waidhi DMV. (Picha zote kwa hisani ya swahilivilla.blogspot.com)
   
Rais Mustaafu Ali Hassan Mwinyi akiwa na Mkewe  katika tamasha la kiswahili pamoja na sherehe ya blog ya Vijimambo
Rais Mustaafu Ali Hassan Mwinyi na mkewe wakiwa katika meza kuu pamoja na viongozi wa tamasha hilo
Wanafunzi darasa la kiswahili DMV wakiingiaa ukumbuni tayari kwa kufungua ukumbi kwa nyimbo ya taifa ilioimbwa na watoto hao
Wanafunzi darasa la kiswahili DMV  wakiwa na walimu wao mstari wa nyuma wakiimba wimbo wa taifa na kumkaribisha mgeni rasmi ambae ni  Rais Mustaafu Ali Hassan Mwinyi pamoja na mkewe
Wageni kutoka sehemu mbali mbali nchini Marekani wakiwa wamesimama kidete kwa heshima ya wimbo wa taifa wa Tanzania ulioimbwa na wanafunzi darasa la kiswahili DMV
Meza kuu ya viongozi waalikuwa wakiwapigia makofi wanafunzi darasa la kiswahili DMV baada ya kufungua tamasha hilo kwa mwimbo wataifa wa Tanzania.
Mmiliki wa blog ya Vijimambo Luke Joe akitoa hotuba kuelezea mafanikio ya blog yake ambayo imeshika hatamu hapa DMV na kua blog imara inaowaunganisha waTanzania wanaoishi hapa DMV.
Kaimu Balozi Mama Lily Munanka akitoa maelezo mafupi ya Tamasha la kiswahili na kumkaribisha Mgeni Rasmi katika sherehe hizo.
Rais Mustaafu Ali Hassani Mwinyi  akitoa hotuba kuu katika tamasha la kiswahili.
PLAY AUDIO: Ungana nasi kwa kusikiliza Audio ya Hotuba ya Rais Mustaafu Ali Hassani Mwinyi aliyoitoa katika tamasha la kiswahili
 

Baadhi ya waTanzania mbali mbali wakisikiliza hotuba ya Rais Mstaafu Ali Hassani Mwinyi.

PICHA ZA USIKU WA VIJIMAMBO 
 Kwa picha zaidi usikose kututembelea tena ukurasa huu huu tunachukua mapumziko kazi ni ngumu mno  pitia baadae ..!!

No comments:

Post a Comment