Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, July 12, 2013

WAFAHAMU SOMJO DJ WATAALAMU WA KUKODISHA VYOMBO VYA MUZIKI NA AJIRA WANAZOTOA KWA VIJANA.

 
 Hawa ni baadhi ya vijana wa SOMJO DJ wakiwa kazini na hawa ni ambao wapo katika kikundi cha sarakasi.

SOMO DJ entertainment ya mjini Moshi ilianzishwa mwaka 1996 na vijana wawili ambao ni Athumani Mganga maarufu kama Somjo na Ramadhani. Vijana hawa walikua na ndoto ya kuhakikisha wakazi wa mji wa Moshi wanapata burudani na pia wanakua mfano mzuri wa kuigwa na vijana wengine kwa kuamua kujiajiri wenyewe. SOMJO DJ wameendelea kufanya vizuri sana katika burudani na pia wameweza kuongeza ajira kwa vijana zaidi ya ishirini ambao wamekua wakijipatia kipato kupitia kazi mbalimbali ambazo zimekua zikisimamiwa na SOMJO Dj katika matamasha mbalimbali wamekua wakitoa nafasi kwa vikundi vya sarakasi, dancers, Dj’s, presenters, na wengine wengi.
SOMJO DJ kwa sasa wanamiliki Vyombo vya mziki (Sound System) vyenye dhamani ya zaidi ya milioni hamsini ikiwa ni Generator tatu, Sound system kubwa mbili na Sound system ndogo moja, pia wana Stage/Jukwaa moja kubwa lenye uwezo wa kugawanywa na kutoa majukwaa matatu. Na pia SOMJO DJ wanaifurahia sana kazi yao na wanasema kazi hii ni nzuri kama mtu atakua makini kuifanya ila ni kazi mbaya kama mtu atakua anaifanya bila kuwa makini maana ni kazi ambayo inakuweka karibu sana na pombe na warembo, kwa maana hiyo usipokua makini utajikuta maisha yako yanakosa muelekeo na kuishia kwenye pombe na warembo.

GRARAMA ZA KUKODISHA VYOMBO VYA MUZIKI
*Vyombo vya mziki (Sound System) bei ni kuanzia laki moja (Tshs. 100,000) hadi milioni moja (Tshs. 1,000,000)
*Stage (Jukwaa) laki moja (Tshs. 100,000) hadi laki tano (Tshs.500,000)
Kwa yeyote anayehitaji vyombo vya mziki (Sound System) au Stage (Jukwaa) apige namba hizi 0715 882 373 au 0767 882 373.
 Athumani Maganga almaarufu Somjo akiwa anaweka mitambo sana muda mchache kabla ya kazi kuanza.
 
MAFANIKIO YA SOMJO DJ
*Athumani Mganga ambaye ndie kiongozi na msimamizi wa SOJMO DJ amefanikiwa kujenga nyumba kubwa (self container) yenye sebule, jiko, store na vyumba vinne vya kulala (four bed rooms) chumba kimoja kikiwa ni master bed room.
*Na pia ameshanunua kiwanja (plot) nyingine na tayari amenunua vifaa vya ujenzi (materials) na wiki ijayo anatarajia kuanza shuhuli za ujenzi wa nyumba ya pili.
*Na kwa sasa tayari anamiliki gari aina ya Toyota Hiace.
*Wamefanikiwa kukutana na kufahamiana na watu mbalimbali kutokana na kazi wanazozifanya.
*Na baadhi ya mampuni ambayo SOMJO DJ wameshafanya nazo kazi ni Serengeti Breweries, VodaCom, TBL, TiGo, Star Times, TPC, Redds, na mengine mengi.
Hii ndio nyumba ya Athuman a.k.a Somjo aliyofanikiwa kuijenga kupitia kipitia kazi yake ya kukodisha vyombo vya muziki (Sound System)

 CHANGAMOTO
*Changamoto wanazokutana nazo mara nyingi ni pale wanapopewa kazi na mtu ambaye sio muhusika (dalali) wakati wa makubaliano wanakubaliana vizuri lakini wanapoenda kwenye eneo la kazi wanakuta kazi ni tofauti na walivyokubaliana. Na unakuta dalali amechukua hela nyingi kwa mteja alafu anawalipa SOMJO DJ hela kidogo tofauti na ukubwa wa kazi yenyewe.

MATARAJIO YA SOMJO DJ
*Matarajio ya vijana hawa ni kuwa na vyombo vya muziki (Sound System) na Jukwaa (Stage) ambavyo vyombo vyote hivyo wanatarajia viwe na dhamani ya milioni mia moja au zaidi.
*Na pia wanatarajia kuanzisha mashindano ya u’DJ (DJ’s competition) kwa mkoa wa Kilimanjaro ili kuweza kuwapata na kuwasaidia vijana wenye uwezo wa kufanya kazi ya u’DJ.

            MAFUNZO NA AJIRA KWA VIJANA
*SOMJO DJ wanatoa mafunzo kwa kijana yeyote mwenye kuhitaji kujifunza kazi ya kufunga vyombo vya muziki (Sound System), kuwa MC au Presenter, kuwa DJ, na mafunzo hayo yanatolewa bureeeee….. ila kinachotakiwa na kijana awe na akili timamu, awe anajitambua na pia awe makini katika mafunzo/kazi.
Kwa kijana yeyote anaye hitaji apige namba hizi hapa 0715 882 373 au 0767 882 373.
siku zote hakuna mafanikio yanayokuja kirahisi. Hapa ni Athuman akiandaa box la speaker ili aweza kulipiga rangi.
Hapa kazi imekamilika na speaker zipo tayari.


No comments:

Post a Comment