Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, October 31, 2013

VIJIJI VITANO VINATARAJIA KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI UNAOTARAJIWA KUTEKELEZWA NA SERIKALI YA UJERUMANI

MOSHI wananchi wa vijiji vitano vya tambarare vilivyopo  wilaya ya Moshi wanatarajia kunufaika na mradi mkubwa wa maji ambao unatarajia kuanza kutekelezwa na serikali ya Ujerumani kupitia shirika lake la AKO kwa gharama ya shilingi milioni mia nane na kumi (810,000,000/=) za kitanzania.
 
Makamu mwenyekiti wa AKO Bw. Klaus Boehme amesema asilimia sabini na tano ya utekelezaji wa mradi huo  utagharamiwa na na serikali ya Ujerumani na asilimia 20 klabu ya rotary za Tanzania na Ujerumani na asilimia tano wananchi wa vijiji hivyo vitano.
 
Bw. Boehme ameyazungumza  hayo wakati wa uzinduzi wa mradi huo baada  kutembelea chanzo cha maji cha mananga kilichopo katika mto Ghona ambapo ndipo mradi huo wa maji unatarajiwa kuanza, na aliendelea kusema kuwa vifaa kwaajili ya ujenzi wa mradi huo tayari vimekamilika.
 
Mratibu wa mfuko wa maendeleo ya jamii Mkoani Kilimanjaro (TPP Trust) utakao simamia utekelezaji wa mradi huo wa maji Bw. Sindibadi Mlaki amesema baada ya kukamilika mradi huo utakabidhiwa kwa jumuia ya watumia maji wa vijiji hivyo vitano vya kata ya kilema kusini.
 
Akipokea mradi huo kwa niaba ya serikali katibu tawala wa wilaya ya Moshi Bi. Remida Ibrahimu amewataka wananchi wa vijiji hivyo kuwa walinzi wa mradi huo ili uwe endelevu kwa faida yao na vizazi vijavyo.
 
Vijiji vitakavyo nufaika na mradi huo ni pamoja na  kilema pofu, kilema chini, kilototoni, masaera na kijiji cha masae kyura.

No comments:

Post a Comment