Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, May 15, 2014

JALALA LA KIBAONI LAZIDI KUHATARISHA AFYA ZA WAKAZI WA ENEO HILO

Jalala lililopo Kibaoni Linalolalamikiwa na wakazi wa eneo hilo.


WAKAZI wanaoishi mtaa wa Kibaoni Boman'gombe wilayani hai mkoani Kilimanjaro wameelezea kero na madhara wanayoyapata kutokana na jalala lililopo karibu na makazi ya watu kuwa kero na hatari kwa afya zao.

Wakizungumza na muandishi wetu  ambaye alifika eneo hilo  leo majira ya mchana kuhusu kero ya jalala hilo ambalo linaweza kuzusha magojwa  mbali mbali ikiwamo kipindu pindu na majonjwa ya mlipuko.

Wakazi wa eneo hilo walisema wanapata shida  kutokana na harufu mbaya kutokana na mvua kunyesha pia inzi wamekuwa wengi, pamoja na moshi unaotoka kwenye jalala hilo ambao usababisha majonjwa ya kukohoa kila wakati.

Mkazi mmoja ambaye hakutaka jina lake litajwe alisema kuwa harufu mbaya kuzagaa kwa takataka hasa mifuko ya rambo na inzi hulazimika kula chakula uku wakiwa wamefunga milango na madirisha.

"Tunapata shida sana hasa kipindi hichi cha mvua za masika harufu kali hutoka kwa wingi na inzi wengi wanafumuka jambo ambalo ni hatari kwa afya zetu tunaomba Halmashauri watafute shehemu nyingine ya kumwaga taka mbali na makazi ya watu"

Nae mkazi mwingine alisema kuwa >> "Wanaoathirika zaidi ni watoto ambao ni rahisi kupata majonjwa dawa  wanazopulizia kwenye maeneo wanayoishi kwa ajili ya kuua inzi haikidhi maitaji kwani huwa wanarudi baada ya muda mfupi"

Diwani wa Kata hiyo ya Hai Mjini Jafar Kiure alisema kuwa wameshapeleka malalamiko    hayo kwa Mkurungenzi Melzedeck Humbe lakini hadi sasa jambo hilo halija shudhulikiwa ambapo aliwataka waandishi wa habari kumuuliza Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Clement Kwayu kuhusu jambo hilo.

Akizungumza jambo hilo Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Clement Kwayu alisema kuwa yupo safarini Tanga pamoja na Mkurugenzi wa Halmashauri na kwamba  jambo hilo watalishudhulikia ili kutatua kero hiyo ili wananchi waishi kwa amani.

No comments:

Post a Comment