Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, August 21, 2014

WATANZANIA WASHAURIWA KUJIENDELEZA KIELIMU KWA KUPITIA VYUO VIKUU HURIA

Wananchi, watumishi wa umma na mashirika binafsi  hapa nchini Tanzania wameshauriwa kujiunga katika vyuo vikuu huria vilivyopo hapa nchini ili waweze kujiongezea elimu itakayo wawezesha kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi  sambamba na kumudu ushindani wa soko la ajira.

Rai hiyo imetolewa na rais wa wanafunzi wa chuo kikuu huria cha mjini Moshi Bw. Adinani Kingazi ,walipotembelewa chuoni hapo na makamu mkuu wa chuo kikuu huria cha Tanzania Bw. Tolly Mbwette, ambapo amesema jamii inatakiwa kutambua kuwa ,kuna umuhimu wakujiendeleza kielimu.

Bw. Kingazi alisema njia pekee ambayo itakayoweza kumkomboa mtumishi wa umma ama sekta binafsi kukabiliana ipasavyo katika soko la ajira ni kusoma katika chuo kikuu huria, ambapo kinampa fursa ya kusoma bila kuathiri shughuli zake za kiutendaji.

 Makamu mkuu wa chuo kikuu huria nchini Bw. Tolly Mbwette alisema serikali imeanza kuboresha baadhi miundombinu ikiwemo majengo katika vyuo vikuu huria hapa nchini pia katika kutekeleza mpango wa matokeo makubwa sasa ina mpango maalumu wa kuhakikisha  kuwa inajenga vyuo vikuu huria nchi nzima.

No comments:

Post a Comment