Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, August 27, 2014

ZAIDI YA MILIONI 120 ZINAHITAJIKA ILI KUFANIKISHA “Mount Kilimanjaro Festival”




KILIMANJARO zaidi ya Shilingi Milioni 120 zinahitajika ili kukamilisha Tamasha la Biashara, Utamaduni na Michezo (Mount Kilimanjaro Festival) linalotarajiwa kufanyika Desemba 17-23 mwaka huu mkoani Kilimanjaro.


Pia Mkuu huyo wa Mkoa aliongeza kusema katika ufunguzi wake mwaka huu watakuwa na msanii maarufu wa nyimbo ambaye hakutaka jina lake litajwe na timu ya daraja la kwanza au Ligi kuu itayoweza kutoa burudani kwa ajili ya kuhamasisha wakazi wa mkoa wa Kilimanjaro.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Maandilizi ya Tamasha hilo  Patrick Boisafi alisema Desemba 17-23 ni kilele cha shughuli nzima itakayoanza kufanyika katika wilaya nane za mkoa wa Kilimanjaro ili kutafuta vikundi na timu mbalimbali.

“Kibiashara tamasha hili litasaidia kukuza uchumi, utamaduni na michezo, pia vitatoa hamasa kwa vijana chipukizi lakini litahusisha vikundi na timu za serikali za mitaa, ili kunogesha zaidi, hivyo maandalizi yanatakiwa kuanzia wilayani hadi siku ya kilele”.

Aidha alisema vikundi na timu hizo zinatakiwa kuandaliwa ipasavyo ikiwemo michezo ya bao, ngoma, kukimbia kwa magunia, kuvuta kamba, mpira wa pete, mpira wa miguu na mpira wa wavu.

Kauli mbiu ya Mt. Kilimanjaro Festival ni “ Biashara, Utamaduni na Michezo, kujenga uchumi wa Kilimanjaro”.
Na Jabir Johnson

No comments:

Post a Comment