Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, September 10, 2014

WENYEVITI WA VIJIJI 37 WAMTAKA WAZIRI WA MALIASILI NA MISITU AWAREJESHEE ENEO LA MLIMA KILIMANJARO

MOSHI wenyekiti wa vijiji 37 vinavyozunguka hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, wamepanga kumuona waziri wa Maliasili na Misitu, Mhe. Lazaro Nyalandu, ili aweze kuona umuhimu wa kuwarejeshea wananchi hao eneo la msitu wa Nusu Maili, ili waweze kuulinda msitu huo usiendelee kuharibiwa kama ambavyo unafanyika sasa.

Akizungumza na waandishi wa habari, kwa niaba ya Wenyeviti hao, Mwenyekiti wa Mtandao wa vijiji 37, KIHACONE, Boniface Mmbando amesema wananchi  hao wamepanga kwenda kumuona waziri Nyalandu, wakimtaka kuwarejeshea msitu huo kwa wananchi kwani wao ndio walinzi wakubwa wa rasilimali hizo.

Amesema hali ya uharibifu wa mazingira katika wilaya ya Moshi unatisha kutokana na watu kuendelea kukata miti hovyo, na kwamba kama jitihada za makusudi hazitachukuliwa kwa haraka kuna hatari kubwa ya kukumbwa na jangwa.

Mmbando amesema lengo la kuanzishwa kwa Mtandao huo ni kudhibiti hali ya uhalibifu wa mazingira ambao unafanyika ndani ya hifadhi ya Mlima Kilimanjaro, lakini wanashindwa kutekeleza majukumu yao kutokana na vitisho ambavyo wamekuwa wakivipata kutoka kwa KINAPA.

No comments:

Post a Comment