Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, October 22, 2014

Jumla ya watoto laki tano mkoani Kilimanjaro wanatarajia kupatiwa chanjo ya Surua na Rubella

KILIMANJARO jumla ya watoto laki tano, wenye umri wa miezi tisa hadi miaka 15, mkoani Kilimanjaro, wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya Surua na Rubella, katika wiki ya chanjo hiyo iliyoanza Oktoba 18 na inatarajiwa kumalizikia oktoba 24 mwaka huu.

Akizungumzsa na waandishi wa habari mkoni Kilimanjaro, Meneja Mpango wa chanjo Taifa, Dkt Dafrossa Lyimo, amewataka wazazi, walezi pamoja na wataalamu wa afya kuhakikisha malengo ya serikali ya kuwapatia chanjo watoto hayo yanafanikiwa kwa kiwango kikubwa.

Dkt Lyimo amewataka wazazi hao kuacha tabia ya kuwazuiwa  watoto wao, wasipatiwe chanjo hiyo,  kwa dhana ya kuwa watoto hao wataua kizazi chao.

Alisema kuwa ugonjwa Surua na Rubella ni ugonjwa hatari, kwani huambukizwa kwa njia ya hewa, na kwamba hauna tiba kamili hivyo tiba yake ni kuwahi kupatiwa chanjo hiyo mapema.

Kwa upande wake Mratibu wa Chanjo mkoa wa Kilimanjaro, Dkt Peter Kihamia alisema takwimu zinaonesha kuwa jumla ya watu watatu wamebainiki kuwa na ugonjwa wa Rubella kwa mwaka huu, kati ya vipimo 48 vilivyofanyiwa uchunguzi mkoani Kilimanjaro.

Alisema kwa kipindi cha mwaka jana watu wapatao 28 wilayani Rombo waligundulika kuwa na dalili za ugonjwa wa Rubella, na baada ya kugundua dalili hizo walizitibu.

No comments:

Post a Comment