Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, November 19, 2014

Afungwa jela maisha kwa kosa la kumlawiti mtoto wa miaka saba

 
KILIMANJARO hakimu  mkazi mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Rombo mkoani Kilimanjaro, Naomi Mwerinde, amemhukumu  Evarist Arobogast (24) kifungo cha maisha  jela baada ya kukutwa na kosa la kumlawiti mtoto wa miaka saba na kumuumiza vibaya sehamu za siri.

 Hakimu mwerinde alisema mshtakiwa huyo mkazi wa kijiji cha kirongo juu wilayani Rombo atatumikia kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti mtoto wa miaka saba.

Mwendesha mashtaka wa Polisi, Raymond Sikukuu aliieleza mahakama kuwa mshtakiwa  alimvamia na kumlawiti mtoto huyo wa miaka saba  na kumuumiza vibaya sehemu za siri.

Sikukuu alidai kuwa mnamo tarehe 24 machi mwaka huu katika kijiji cha kirongo juu Usseri ambapo mtoto huyo alifanyiwa kitendo hicho cha kikatili na kumsababishiwa maumivu makali sehemu zake za siri.

Mwendesha mashtaka huyo alisema mtuhumiwa alitenda kosa hilo kinyume cha sheria ya 154 sura 16 ya kanuni ya sheria ya adhabu iliyofanyiwa marekebisho  mwaka 2002.

Akitoa hukumu hiyo hakimu Mwerinde alisema  kuwa baada ya kusikiliza ushahidi wa pande zote  mbili upande wa mashtaka umeweza kuthibitisha shtaka hilo pasipo kuacha shaka.

Hakimu huyo alisema  pia maelezo ya daktari yaliyowasilishwa mahamani hapa  imeonesha kuwa mtoto huyo alifanyiwa kitendo hicho cha kikatili.

Hakimu Mwerinde alisema  kuwa vitendo vya ubakaji na ulawiti katika wilaya ya Rombo vimeshamiri kwani katika mahakama hiyo zipo kesi nyingi za kulawiti.

Alisema  kuwa kutokana na hali hiyo mshtakiwa atatumikia kifungo cha maisha jela ili iwe fundisho kwake na kwa watu ambao wamekuwa wakifanya vitendo hiyo kwa watoto wadogo.

No comments:

Post a Comment