Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, November 24, 2014

Serikali imelenga kuhakikisha kuwa kaya zote hapa nchini zinajiunga na bima ya afya

KILIMANJARO waziri wa Afya na Maendeleo ya Jamii, Dkt. Seif Rashid, amesema serikali imelenga kuhakikisha ya kuwa kaya zote hapa nchini zinajiunga na bima ya afya ili kujikinga na majanga yanayotokana na kuugua au ajali.

Dkt. Rashid ameyasema hayo wakati wa hafla ya kuuzindua mfuko wa bima ya afya ya jamii ulioboreshwa, (iCHF), kwa Mkoa wa Kilimanjaro, iliyofanyika wilayani Siha.

Katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Mganga mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Dkt. Mtumwa Mwako, Dkt. Rashid amesema serikali iko katika hatua za mwisho kuupeleka mswada bungeni ambao utalazimisha kila kaya ijiunge katika bima ya afya.

Aidha amesema kuwa serikali inafahamu changamoto zilizoko kwenye huduma za afya hapa nchini na kwamba kwa kutambua hilo, imekuwa ikifanya juhudi mbalimbali ili kuhakikisha inakabiliana na changamoto hizo.

Dkt. Rashid ametoa shukrani zake za dhati na zile za serikali kwa shirika lisilo la kiserikali la nchini Uholanzi la PharmAccess kwa mchango wake mkubwa iliyotoa na inayoendelea kuutoa katika kuiboresha sekta ya afya hususan katika kuuboresha mfuko wa afya ya jamii, (iCHF).

Akizungumza katika hafla hiyo kwa niaba ya Mkurugenzi mkuu wa mfuko wa bima wa Taifa, (NHIF), Mkurugenzi wa iCHF,  Athuman Rehani, amesema NHIF imekasimiwa na serikali mamlaka ya kusimamia mfuko wa afya ya jamii ulioboreshwa, lengo likiwa ni kuboresha afya ya jamii nchini.

Amesema mfuko wa Taifa wa bima ya afya umelenga ifikapo mwaka 2015 asilimia 30 ya watanzania wotw watakuwa wamejiunga na bima ya afya.

Ameongeza kuwa katika kipindi cha Septemba mwaka huu asilimia 16.5 ni wanzania pekee ambao wanatumia biha hiyo.

Kwa upande wake  Mkurugenzi wa Utetezi na utafutaji rasilimali wa PharmAccess,  Kwasi Boahene, amesema kutokana na mafanikio yaliyoonekana wilayani Siha, Shirika hilo limelenga kupanua wigo wa huduma zake kwa wilaya zote za Mkoa wa Kilimanjaro na Mikoa ya jirani ya Arusha na Manyara.

Nae afisa masoko wa Shirika la PharmAceess Edga Masatu amesema kuwa bima hiyo itasaidia jamii kuondokana na dhoruba ya gharama kubwa za matibabu ambazo zilikuwa zikitolewa na hivyo kusababisha wananchi wengi kushindwa kumudu gharama za matibabu.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Siha Rashid Kitambulilo, amesema mpango huo umekuwa na mafanikio makubwa ambapo jumla ya familia 431 wamejiunga na iCHF.

No comments:

Post a Comment