Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, November 24, 2014

Serikali yatakiwa kuingilia kati tatizo la ulevi wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro

KILIMANJARO serikali imetakiwa kuingialia kati tatizo la ulevi wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro  kutokana na tatizo hilo kuendela kushamiri na kuathiri nguvu kazi ya taifa ikiwa ni pamoja na kuchangia ongezeko la watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu.

Rai hiyo ilitolewa jana na Mwenyekiti wa Asasi ya jinsia na maendeleo wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro (AJIMARO) Athony Massawe, wakati akikabidhi msaada wa chakula kwa watoto yatima na wale wenye maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI katika kituo cha Cornel Ngaleku kilichopo wilayani humo.

Massawe alisema tatizo la ulevi kwa wananchi wilayani Rombo limeendela kukua siku hadi siku na kwamba ni vema serikali ikaingilia kati  na kulidhibiti, kwani limechangia maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI na kusababisha ongezeko la watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu.

Aidha tatizo hilo limechangia kiwango cha umasikini kuongezeka kwa wananchi wa wilaya hiyo kutokana na vijana wengi ambao ndio nguvu kazi kuathiriwa na pombe hizo kali  na kusahau kufanya kazi kwa ajili ya kujileta maendeleo na kuondokana na hali ya umasikini.

Massawe alisema kutokana na tatizo hilo asasi hiyo imejikita katika utoaji wa  elimu kwa wananchi juu ya adhari za ulevi ikiwa ni pamoja na namna ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa wa UKIMWI ili kuinusuru jamii hiyo.

Katika hatua nyingine Massawe aliitaka jamii, taasisi mbalimbali za kiserikali na zisizo za kiserikali kuguswa na kuona umuhimu wa  kuwasaidia watoto yatima na wale waishio katika mazingira magumu kwani wamekuwa wakikabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa chakula.

Awali akizungumza wakati akikabidhiwa msaada wa chakula hicho Sista Ritha Massawe alisema kituo hicho kinakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa chakula kwaajili ya watoto kutokana na wafadhili wengi kuacha kutoa misaada kutokana na hali ya uchumi kuwa mbaya.

Alisema kwa sasa watoto yatima wengi wameongezeka ikiwa ni pamoja na wale wanaoishi katika mazingira magumu hali ambayo inachangiwa na  ukosefu wa malezi  bora kutoka kwa  wazazi wao kutokana na  kuendekeza ulevi  hivyo kusahau wajibu wao muhimu.

Alisema wazazi wengi wameathiriwa na ulevi jambo ambalo limekuwa likiwaathiri  watoto ndani ya familia na kupelekea watoto kutoroka majumbani na kuishi mitaani na kukosa mahitaji muhimu kama chakula, elimu, mavazi na malezi bora.

Kwa upande wao baadhi ya wananchi wilayani Rombo walisema kwasasa wanawake ndio wanaofanyakazi kutokana na vijana na wanaume kushindwa kufanyakazi kwaajili ya kujiingizia kipato na kwamba wengi huishia vijiweni wakivuta dawa za kulevya na kutumia pombe kali.

No comments:

Post a Comment