Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, December 29, 2014

Wadau wa elimu wailalamikia serikali kwa kubadili viwango vya ufaulu mara kwa mara

KILIMANJARO wadau wa elimu mkoani Kilimanjaro wameilaumu serikali kwa kubadilisha mara kwa mara viwango vya ufaulu bila kufanya tathimini ya kutosha, mpango uliofananishwa na  upanuzi wa magoli ili kumwezesha kila mchezaji kufunga kirahisi.
 
Lawama hizo zilitolewa hivi karibuni na Mkuu wa Shule ya Sekondari Majengo iliyo chini ya Kanisa Katoliki Jimbo la Moshi, Peter Lyimo, katika hotuba yake kwenye mahafali ya 28 ya wahitimu 568 wa kidato cha nne.
 
Alisema kuwa, hali hiyo ni ya hatari na inaua elimu na taifa haliwezi kuendelea kwa mfumo huo na kushauri serikali kuiboresha elimu ili iweze kuandaa wanafunzi kuweza kujitegemea.
 
Aliitaka serikali kuziboresha shule za ufundi na kuzipa msukumo wa pekee, akiamini kuwa ni muhimu kwani zinawezesha kuzalisha kazi badala ya kufatufa kazi.
 
Mkuu huyo shule, alisema elimu ya Tanzania haiwezi kuwa bora kama wananchi hawataimiliki kwa mchango na uwajibikaji na kuongeza kuwa, kama taifa na jamii yanahitajika mabadiliko ya kifikra na kimtazamo kuhusu elimu.
 
“Ndugu zangu, tunatakiwa kuchangia elimu yetu ili iwe bora, kuna wanafunzi wengi ambao wanashindwa kusoma kutokana na kukosa msaada, tunakumbuka kwamba kila mmoja wetu hapa amefika alipo kwa kutembea mgongoni mwa mtu mwingine…baba, mama, mjomba, shangazi na wengineo,” alisema. 
 
Chanzo: Tanzania Daima

No comments:

Post a Comment