Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, March 7, 2015

Mtoto huyu alieteseka kwa miaka saba akiwa anakula chakula katika chombo kimoja na Mbwa, Paka na Kuku

KILIMANJARO mtoto wa kike anayekadiriwa kuwa na umri kati ya miaka kumi na tano na kumi na sita (15-16) anayeishi katika kitongoji cha Ngundeni,  kijiji cha Tela, kata ya Machame Narumu, wilayani Hai Mkoani Kilimanjarao ameishi kwa kufungwa na kamba migombani kwa miaka saba huku akila chakula na Mbwa, Paka na Kuku wanao pita eneo hilo.

Tukio hilo la aina yake limewashtua wakazi wanaoishi kijijini hapo wilayani Hai kutokana na mtoto huyo kutoweka ghafla kwa kufichwa na Bibi wa upande wa baba na baadae kuonekana tena katika hali iliyo jaa ukatili wa kutisha.

Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti wa Dawati la watoto na jinsia wilaya ya Hai, Happy Eliufoo alisema kuwa mtoto huyo aligundulika kutokana na msamaria mwema aliye muona mtoto huyo kafungwa katika shina la mgomba  na kamba miguuni huku akila chakula katika mazingira yasiyo ridhisha hivyo kuamua kutoa taarifa katika kituo hicho.

Alisema kuwa kwa taarifa za awali mtoto huyo ambaye ni yatima anayeishi na bibi yake alikuwa akisoma na wenzake ambapo alifika darasa la tatu kisha kutoweka ghafla ambapo baada ya kupatikana katika hali hiyo walio kuwa wanafunzi wenzake walipigwa na butwaa.

Mtoto huyo hutolewa asubuhi na kufungwa mgombani ambapo bibi yake huendelea na  shughuli zake za kila siku huku jua na mvua zikimuishia akiambulia kula chakula kilicho wekwa katika ndoo iliyo katwa na inapo timia majira ya usiku mara baada ya byake kurudi katika kazi zake hutolewa na kufungwa ndani karibu na ng’ombe na Mbuzi.

Eliufoo aliongeza kuwa kitendo cha mtoto huyo kufichwa shambani huko kumempelekea mtoto huyo kuathirika kisaikolojia kwani mpaka kwa sasa hapendi kuangalia watu usoni na hata kuongea inampa shida.

Akielezea hali ya kuishi kwa mtoto huyo bibi yake aliye jitambulisha kwa jina la Anthonia Ngowi alisema kuwa aliamua kuishi na mjukuu wake huyo baada ya baba yake  na mama yake  kufariki mwaka 2009.

“Mtoto huyu ni mkorofi sana kwa hali hiyo hunilazimu kumfunga na kamba kwani hujisaidia kisha kupaka haja kubwa ndani” alisema bibi yake.

Alipo hojiwa zaidi juu ya kumfunga Mtoto huyo karibu na mifugo hiyo huku akijua wazi kuwa ni kosa kumfanyia mtoto vitendo vya ukatili bibi huyo alidai kuwa huwa anafanya hivyo ili kuzuia mifugo yake kuibiwa na wezi hivyo mtoto huyo kutumika kama mlinzi.

Awali akitoa ufafanuzi wa ukatili huo bibi huyo alidai kuwa mtoto huyo kabla ya kufiwa na baba yake aliugua ugonjwa wa degedege hivyo kupelekwa kwa mganga wa jadi ambapo bibi huyo alisema kuwa alipona ila mganga huyo hakumaliziwa pesa yake ambayo ni kiasi cha elfu thelethini ndipo ugonjwa huo ulipo mrudia tena.

“Kweli nasema ukweli kuwa ndiyo sababu ya mtoto huyu kuwa hivi mimi siyo mshirikina na wala siyo mchawi nimemfungia mtoto huyu miaka saba shambani kwani sikupata msaada toka kwa ndugu zangu hata kwa watoto wangu” alidai bibi huyo.

Kwa upande wake mwenyekiti na mwanaharakati washirika lisilokuwa lakiserikali linalo jihusisha na utetezi wa wanawake na watoto Messe Ndossi alisema kuwa jambo hilo kwa wilaya ya Hai ni lakusikitisha licha ya elimu kutolewa kila siku juu ya haki ya mtoto na malezi yaliyo bora.

“kwa kweli bado tunahitaji kutoa elimu hasa vijijini kufichua unyama na ukatili unaotendeka kwa watu wasio kuwa na sauti kama hawa ili kuweza kujenga kizazi ambacho siyo tegemezi siku za baadae, hivyo kila mmoja aweze kutimiza wajibu wake kwa kupinga ukatili” alisema Ndossi.

Aliongeza kuwa jamii inatakiwa kutojihusisha na imani za kishirikina kwani kwa kufanya hivyo wanajikuta wakifanya ukatili kwa watu wasiyo kuwa na hatia, huku akihusisha tukio hilo na imani za kishirikina.

Mtoto huyo alichukuliwa nakupelekwa hosipitali ambapo alibainika kuwa na ugonjwa wa "UTI" kisha kupatiwa matibabu na kupelekwa katika kituo cha kulelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu kwa uangalizi wa karibu,  huku bibi yake akishikiliwa kwa mahojiano zaidi juu ya tuhuma za kumfanyia mtoto ukatili huo.

Uelewa wa masuala ya ulinzi kwa mtoto wilaya ya Hai utafiti ulibani kuwa ni 85%, pamoja na uelewa wa jamii kuwa juu kiasi hicho lakini bado kuna tatizo kubwa la ukiukwaji wa haki za watoto hali inamaanisha kuwa ama jamii inapuuzia jambo hili au tabia na mitazamo haijabadilika licha ya kuelewa.

Tafsiri yake ni kwamba, juhudi zinahitajika kuweka mikakati ya makusudi kuanzia ngazi ya familia, Kitongoji, Kijiji, Kata, Wilaya hadi Taifa kuhusu ukatili dhidi ya watoto.

No comments:

Post a Comment