Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, June 27, 2015

Watiania wa CHADEMA Moshi vijijini warudisha fomu za kuwania ubunge na udiwani

Mwenyekiti wa Chadema Jimbo la Moshi vijijini,Godlisen Maramia akipokea fomu kutoka kwa Deogratius Mushi ya kuwania nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi vijijini wakati aliporudisha katika ofisi za chama hicho zilizopo Majengo.
Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Moshi vijijini ,Godlisen Maramia akimpongeza mtia nia Deuogratius Mushi kwa uamuzi wa kuingia katika kinya’ng’anyiri cha kuwania nafasi hiyo.

Mushi akipongezwa na makada wengine wa Chadema waliofika kumsindikiza ofisnini hapo.

Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Moshi vijijini,Godlisen Maramia akipokea fomu toka kwa Tally Kisesa ya kuwania Ubunge wa viti maalumu katika jimbola Moshi vijijini.

Mtia nia wa nafasi ya Udiwani katika kata ya Kindi,kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Michael Kirawira akirejesha fomu ya kuwania nafasi hiyo katika ofisi ya Chadema kata ya Kindi.



Wananchi wa kata ya Kibosho Magharibi wakimlaki Mgombea wa nafasi ya Ubunge Deo Mushi ambaye pia ametangaza kuwania nafasi ya Udiwani katika kata hiyo.

Mgombea wa nafasi ya Ubunge katika jimbo la Moshi vijijini,Deogratius Mushi,akitia saini katika kitabu cha wageni mara baada ya kuasili katika kata hiyo.

Deo Mushi ambaye pia ni mwenezi wa Chadema wilaya ya Moshi vijijini ,akizungumza na baadhi ya wananchi katika kata ya Kibosho Magharibi .

Baadhi ya wananchi waliohudhuria kikao hicho.

Deo Mushi akizungumza.


Mbali na kuwania nafasi ya Ubunge, Deogratisu Mushi pia amerudisha fomu ya kuwania nafasi ya udiwani katika kata ya Kibosho Magharibi na hapa akikabidhi kwa Mwenyekiti wa Chadema katika kata hiyo Kikas Mmasi.

Mwenyekiti wa Chadema katika kata ya Kibosho Magharibi Kikas Mmasi akizungumza katika kikao hicho mara baada ya kupokea fomu ya Deo Mushi.

Na Dixon Busagaga 


No comments:

Post a Comment