Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, October 21, 2015

LOWASSA AONGOZA MAELFU KUUAGA MWILI WA DK.EMMANUEL MAKAIDI VIWANJA VYA KARIMJEE DAR

Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kupitia mwamvuli wa Ukawa, Edward Lowassa akitoa heshima za mwisho mbele ya jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti Mwenza wa umoja huo, Dk. Emmanuel Makaidi wakati wa ibada ya kuuaga iliyofanyika viwanja vya Karimjee Dar es Salaam leo mchana. Katika ibada hiyo viongozi mbalimbali wa vyama vya siasa na serikali walihudhuria.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye ibada hiyo.
Wananchi wakiwa wamejipanga foleni wakati wakienda kutoa heshima za mwisho kwa marehemu.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Tanzania Bara, Philip Mangula (kulia), akipeana mkono wa pole na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe wakati alipofika kuhudhuria ibada hiyo.

Mjane wa marehemu, Dk. Emmanuel Makaidi, Modesta Ponela akiwa ameinua mikono wakati akimuaga mumewe katika ibada hiyo.
Msajili wa Vyama Vya Siasa, Jaji Francis Mtungi, akizungumza kwa niaba ya serikali wakati wa misa hiyo ya kumuaga Dk. Makaidi.

Lowassa na Sumaye wakiteta jambo katika ibada hiyo.
Mchungaji David David (kulia), akiongoza ibada hiyo.
Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye (katikati), akiwa na viongozi wengine katika ibada hiyo.
Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali wakichukua matukio ya ibada hiyo.
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kupitia mwamvuli wa Ukawa, Edward Lowassa (wa pili kulia), akiwa na viongozi wa Ukawa. Kulia ni Mgombea Mwenza, Juma Duni Haji, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi, James Mbatia.
Waombolezaji wakiwa wamejipanga foleni wakati wa kwenda kutoa heshima za mwisho.
Ibada ikiendelea.
Ndugu jamaa na marafiki wakiendelea na kumuaga Dk. Makaidi.

Ni vilio na huzuni baada ya ibada hiyo ya kumuaga mpendwa wetu Dk. Makaidi.
Jeneza lenye mwili wa Dk. Makaidi likiingizwa kwenye gari tayari kuelekea makaburi ya Sinza kwa mazishi.



Na Dotto Mwaibale

No comments:

Post a Comment