Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa-SUKI Ndg Rabia Abdalla Hamid anatarajia kufanya ziara ya kuzungumza na Makundi mbalimbali ya Kijamii, Taasisi, NGO’s na vyama vya kijamii katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na Njombe, kama ifuatavyo;
1. Tarehe 14/06/2026 Lindi
2. Tarehe 15/06/2026 Mtwara
3. Tarehe 17/06/2026 Ruvuma
4. Tarehe 18/06/2026 Njombe
Makundi ya kijamii ya wakulima, wafugaji, wachimbaji wa madini, wavuvi, wenye mahitaji Maalum, wanavyuo, Vyama vya ushirika, Wajane, Mama Lishe na Baba lishe, Maafisa Usafirishaji (Bodaboda, bajaji, daladala, maguta), vikundi mbalimbali vya wajasiliamali nyote mnakaribishwa kusema changamoto mbalimbali zinazowakabili, CCM ndio kimbilio la Makundi yote ya kijamii, Ndg Rabia Abdalla Hamid atakusikiliza na kutatua kero inayokabili kikundi chochote cha jamii katika jamii.
Aidha, Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuacha Tabasamu kwa kila Mtanzania.

No comments:
Post a Comment