Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameshiriki Maadhimisho ya Miaka 60 ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT) yaliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam tarehe 12 Juni, 2026.
Maadhimisho hayo yamekuwa fursa ya kutafakari mchango mkubwa wa Benki Kuu katika kusimamia uthabiti wa uchumi, mfumo wa fedha na maendeleo ya sekta ya kifedha nchini kwa kipindi cha miongo sita.
Katika kipindi cha miaka 60, Benki Kuu ya Tanzania imeendelea kuwa nguzo muhimu katika kuimarisha uchumi wa taifa, kudhibiti mfumuko wa bei, kusimamia sera za fedha na kuimarisha mazingira ya uwekezaji yanayochochea ukuaji wa uchumi na maendeleo ya wananchi.
Ushiriki wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika maadhimisho hayo unaonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuendelea kuimarisha sekta ya fedha na kujenga uchumi imara, shindani na jumuishi kwa manufaa ya Watanzania wote.


No comments:
Post a Comment