Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, July 27, 2012

MASHINDANO YA OLIMPIKI KUFUNGULIWA LEO NDANI YA MASAA MACHACHE YAJAYO




 
Mwenge wa Olimpiki Ukiwa Umefika Mbele ya Lango la Uwanja Wa Olimpiki Tayari kwa kufunguliwa Masihindano hayo Baada ya Mwenge wa huo Kuzunguka kwa Siku 68 Kuzunguka Uingereza

 

 Macho yote leo ni huko London Uingereza kwenye sherehe za ufunguzi wa Mashindano ya Olimpic 2012
Ufunguzi huo wa saa Tatu ulioandaliwa na mshindi wa Tuzo za Oscar Muongozaji  wa Filamu ya Slumdog Millionaire,  Danny Boyle, Utaangaliwa na Watu 60,000 kwenye uwanja Maalum wa mashindano hayo uliojengwa huko East End, London na kuangaliwa kwenye Luninga na watazamaji zaidi ya Bilioni Moja Duniani Kote.
Sherehe hizo zitarushwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za huko ambapo ni saa sita usiku kwa saa za Afrika Mashariki.
Watazamaji watatakiwwa kuimba pamoja na watumbuizaji  na kutengeneza picha ya  aina yake kwenye tukio hilo kubwa  litakalokaribisha wanamichezo 16000 kutoka nchi 204 duniani.

Kutakua na ulinzi mkali kwenye mashimndano hayo unaotolewa na kampuni ya ulinzi ya G4S

Mamlaka zinazohusika na kukabiliana na ugaidi zimesema hakuna wasiwasi na matukio hayo huku waziri mkuu wa uingereza David Cameroon akisema Olimpiki yenye kilikua kipaumbele chake

No comments:

Post a Comment