CHAMA
cha walimu Tanzania (CWT) kimesema kuwa hakipo tayari kuwatetea walimu
walioenguliwa majina yao katika zoezi la kusimamia Sensa mwaka huu na
kujiandaa kuvuruga zoezi hilo.
Kauli
hiyo ilitolewa jana na Kaimu Katibu wa CWT Taifa Ezekiah Oluoch
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari mjini Tunduma baada ya
kujionea uharibifu wa ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Mji mdogo wa
Tunduma iliyovunjwa siku ya mgomo wa walimu.
Oluoch
alisema kuwa licha ya CWT kuwa na nyaraka za kuenguliwa kwa baadhi ya
walimu katika zoezi hilo, amewataka walimu kushiriki kikamilifu katika
zoezi hilo na kwamba mwalimu ambaye atabainika kuhujumu zoezi hilo
Serikali imshitaki kama mhalifu mwingine.
Akizungumzia
suala la kulipa fidia za uhalibifu wa jengo na wizi wa mali za ofisi ya
Mkurugenzi wa Mamlaka ya mji wa Tunduma uliotokana baada ya wanafunzi
kufika eneo hilo na kudai haki ya kufundishwa siku ya mgomo wa walimu
Juni 30, mwaka huu, alisema CWT haipo tayari kulipa kwasababu hakuna
ushahidi wa moja kwa moja kuwa walimu ndiyo waliohusika na uhalifu huo.
Alisema
uchunguzi wa Serikali ukibaini kuwa kuna walimu waliohusika
kuwashawishi wanafunzi kuandamana mpaka katika ofisi hizo, basi walimu
hao wawajibike wao kama wao na endapo kuna walimu walishiriki moja kwa
moja katika kuvunja ofisi na kuiba mali za ofizi hiyo CWT watalipa na si
vinginevyo.
‘’Ninachoweza
kusema kwa niaba ya CWT ni kutoa pole kwa uongozi wa Mamlaka kwa
kuvunjiwa ofisi na kuibiwa samani na kikundi cha wahuni na tunalaani
tukio lililotokea, lakini kwasababu CWT na ofizi Mamlaka ni majirani
mwema tutakapopata tathimini ya uhalibifu huo tutatoa kifuta machozi
lakini siyo fidia ya ujumla other wise Serikali itupeleke mahakamani’’
alisema Oluoch.
Sanjari
na hayo alisema kuwa Serikali haikitendei haki chama cha walimu kwa
kuwahusisha viongozi wake kuwa wanafadhiliwa na Chadema kwa ajili ya
kuvuruga amani ya nchi na kwamba ikithibitisha suala hilo yeye atakuwa
kiongozi wa kwanza kujiuzulu wadhifa wake na kurudi kufundisha.
Kwa
upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Mji wa Tunduma Aidan
Mwasiga alisema kuwa uhalibifu uliotokea siku ya mgomo wa walimu nchini
CWT hawawezi kukwepa lawama kuwa chanzo cha uhalibifu wa ofisi yake na
wizi na kwamba wala suala hilo halihusiani na Siasa.
Alizitaja
baadhi ya athari kubwa zilizopatikana bada ya ofisi yake kuvunjwa na
kuibwa baadhi ya vitu kuwa ni pamoja na mji huo kukosa ushuru kutokana
na nyaraka zote za kiserikali kuibwa vikiwemo vitabu vya kukusanyia
mapato ya mji huo.
No comments:
Post a Comment