UTANGULIZI...!
Mheshimiwa
Spika, kwa mujibu wa Kanuni za Bunge kanuni ya 99(7),toleo la mwaka 2007 na kwa
niaba ya Kambi Rasmi ya UpinzaniBungeni,napenda kuwasilisha maoni ya Kambi
Rasmi ya Upinzanikuhusu Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Mafungu ya Wizara
yaFedha-Fungu 50 Wizara ya Fedha, Fungu 21 Hazina, Fungu 22 Denila Taifa na
Fungu 23 Ofisi ya Mhasibu Mkuu wa Serikali. Vile vileFungu 10 Tume ya Pamoja ya
Fedha na Fungu 13 Kitengo chaUdhibiti wa Fedha Haramu na Ufadhili wa Ugaidi.
Mheshimiwa
Spika, mafungu
yote yaliyo chini ya Wizara ya Fedhayanaomba kuidhinishiwa na Bunge lako tukufu
jumla ya shilingi Bilioni4,208 (trilioni 4.2) ili yaweze kutekeleza majukumu
yake. Mafunguhaya maombi yake ya Fedha ni sawa na asilimia 28 ya Bajeti nzimaya
Serikali ya mwaka wa Fedha 2012/13.
Mheshimiwa
Spika, Wizara
ya Fedha ndiyo msimamizi mkuu waUchumi wa nchi ikitekeleza majukumu mbalimbali
ikiwemo,kusimamia ukusanyaji wa mapato ya ndani na ya nje, kusimamiamatumizi ya
Serikali, kusimamia utendaji wa Taasisi na Mashirika yaUmma, kusimamia manunuzi
ya Serikali na Taasisi na Mashirika ya Umma, kusimamia Deni la Taifa na dhamana
za Serikali, kutafutasuluhisho na kusimamia mfumo wa kodi wa Serikali ya
Jamhuri yaMuungano na kupambana na Fedha haramu. Sambamba na hayoni kusimamia
na kutekeleza mpango wa kupunguza umasikini nchinikupitia utekelezaji wa
MKUKUTA II.
Mheshimiwa
Spika, Wizara
ya Fedha na mafungu yote yaliyo chiniyake ndio moyo wa Serikali na hivyo ni
lazima kuitazama Wizara hiikwa jicho kali na kutilia mashaka kila jambo ambalo
inalifanya ilikuhakikisha kuwa moyo huu hausimami maana madhara yake nikwa
taifa zima na watu wake. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungenikupitia Waziri Kivuli
wa Fedha inatekeleza wajibu huu kwa Uzalendo,Uadilifu na kwa misingi ya
Uwajibikaji. Tumetekeleza wajibu huu natunaendelea kuutekeleza bila kujali
maneno na kuweka maslahi yaTaifa letu mbele ya kila kitu kingine. Maslahi ya
Taifa ni zaidi yavyama vya siasa, mahala tunapotoka au dini tunazoamini.
Maslahiya Taifa ni kwa ajili ya Watazania na hasa Watanzania milioni 30
(TheBottom 30M) ambao bado wanaishi katika ufukara mkubwa sanawakikosa huduma
muhimu za jamii na wanaoishi vijijini ambapohakuna umeme, barabara hazipitiki
na wanahangaika kutwakutafuta maji safi na salama. Maslahi ya Taifa sio faida
yawachache wenye kuishi mijini au wanasiasa wanaotafuta ushawishikwa umma bila
kujali matakwa ya Umma. Watanzania wanyongewa vijijini wanajua maslahi yao ni
nini. Wanajua kina nani Wanapigania maslahi ya Wanyonge.
- MAPATO YA SERIKALI
Mheshimiwa
Spika, kwa
mujibu wa taarifa ya mwenendo waUchumi ya mwezi Julai (Monthly Economic Review,
July 2012)iliyotolewa na Benki Kuu ya Tanzania, katika kipindi cha mwezi
JuniSerikali iliweza kukusanya kiasi cha shilingi bilioni
998.0.
Hata hivyomatumizi halisi yalikuwa kiasi cha shilingi bilioni1,911.8 haliiliyopelekea
kuwepo kwa nakisi baada ya kuondoa msaada wamasharti wa masharti wa shilingi
bilioni 400.2; nakisi hiyo ililipwa kwavyanzo vya ndani na nje.
Mheshimiwa
Spika, katika
makusanyo hayo ya mwezi Juni Mamlakaya Mapato Tanzania ilikuwa imejiwekea lengo
la kukusanya kiasi chashilingi bilioni 242.4 kama kodi ya Mapato, lakini
ilikusanya kiasi chashilingi bilioni 366.0 kiasi ambacho ni zaidi kwa asilimia
60.8 yamalengo yaliyokuwa yamewe kwa.
Kambi ya
Upinzani inapenda
kulikumbusha Bunge na Taifa kwambakatika Bajeti Mbadala iliyowasilishwa hapa
Bungeni tulisemakwamba TRA wanao uwezo wa kukusanya mpaka shilingi trillionmoja
kwa Mwezi iwapo tutadhibiti misamaha ya kodi, tutakusanyakodi stahili katika
Sekta ya Madini na tutasimama kidete kuzuiaukwepaji kodi wa Makampuni ya
Kimataifa.
Mheshimiwa
Spika, Kambi ya
Upinzani inaitaka Mamlaka ya MapatoTanzania kuimarisha zaidi marekebisho
yanayofanyika katika mfumowa kodi ili kufikia lengo tajwa la kufikia makusanyo
ya zaidi yaasilimia 20 ya Pato la Taifa. Mabadiliko kadhaa tunayoyafanyakwenye
Sheria ya Fedha itakayosomwa hapa Bungeni katikamkutano huu wa Bunge yana lengo
hilo la kupanua wigo wa kodina hivyo kulifanya Taifa lijitegemee.
2.1 Mauzo
ya Nje
Mheshimiwa
Spika, Wizara ya
Fedha kupitia Benki Kuu ya Tanzaniainapaswa kuhakikisha kuwa Akiba ya Fedha za
Kigeni nchiniinakuwa imara muda wote. Biashara ya nje ndio inaingiza Fedha
zakigeni nchini kwa hiyo ni eneo la kutazama kwa makini na kuchukuahatua mwafaka.
Taarifa ya mwenendo wa uchumi kwa mwezi Julaiiliyotolewa na Benki kuu
inaonyesha kuwa jumla ya mauzo yaTanzania nje yalikuwa dola za kimarekani
7,990.0 milioniukilinganisha na kiasi cha dola 7,050.7 milioni kwa kipindi kama
hichokwa mwaka 2011 na hali hii ilisababishwa kwa kiasi kikubwa kutokana na
kuongezeka kwa bei ya mauzo ya dhahabu .
Hatahivyo
Manunuzi yetu kutoka nje yamefikia dola za Kimarekani 12,959milioni.
Mheshimiwa
Spika, , taarifa hiyo inaonyesha kuwa mauzo yadhahabu Nje kwa mwaka 2011 yalikuwa
kiasi cha dola 2,330.7 milioni sawa na aslimia 56.7% ya mauzo yote nje, wakati
mauzo yanje kutokana na bidhaa zilizozalishwa viwandani yalikuwa na jumlaya
dola 922.0 milioni sawa na asilimia 22.4% ya mauzo yote ya nje.Aidha mauzo ya
mazao mbalimbali kama Pamba, Katani, Korosho,Chai, Kahawa na mengineyo yalikuwa
na thamani ya dola 761.1 milioni kwa kipindi hicho cha mwaka 2012.
Mheshimiwa
Spika, taarifa
hiyo imeendelea kuonyesha kuwatuliagiza bidhaa kutoka nje zenye thamani ya dola
za Kimarekanimilioni 12,958.7. Katika manunuzi hayo tuliyofanya mafuta pekeyake
yalikuwa na thamani ya dola za Kimarekani milioni 3,586.1 ambalo ni ongezeko la
asilimia 60.08% ukilinganisha na kipindi kamahicho kwa mwaka 2011.
Mheshimiwa
Spika, takwimu
hizi zinaonyesha kwamba fedha zote zakigeni zilizotokana na mauzo ya dhahabu,
bidhaa za viwandani naKorosho zilitumika kuagiza mafuta pekee yake! Hali hii ni
mbayasana kwa uchumi wa Taifa letu na juhudi zote za kuongeza mauzonje zinaliwa
na uagizaji wa Mafuta ambao umepanda sana katika siku za hivi karibuni.
Kambi
Rasmi ya Upinzani inatambua
kuwa kuanzia mwaka janaSerikali imekuwa ikitekeleza mpango wa Umeme wa
dharuraambao umepelekea matumizi makubwa ya Mafuta. Hata hivyoieleweke kuwa
Mpango mzima wa Manunuzi ya Mafuta yakuendesha mitambo ya Umeme inaligharimu
Taifa Fedha nyingisana. Takwimu zinaonyesha kuwa Serikali inapaswa kutumia
zaidi yashilingi 42 bilioni kila Mwezi kuendesha
mitambo ya dharura yaUmeme. Manunuzi yenyewe ya Mafuta yamejaa mazonge
yaufisadi uliokithiri. Licha ya kutaka Spika aunde timu ya kuchunguzaufisadi
katika manunuzi ya Mafuta na licha ya Kamati ya Bungekutaka Uchunguzi wa
kibunge kufanyika katika manunuzi hayabado hakuna hatua inayochukuliwa.
Kambi
Rasmi ya Upinzaniinaitaka Mamlaka ya Manunuzi ya Umma PPRA kufanya uchunguziwa
kina kuhusu manunuzi ya mafuta kuzalisha Umeme ambayoyanachoma bilioni 42 za
Serikali kila Mwezi. PPRA hapaswi kufumbiamacho manunuzi yanayotafuna shilingi
1.4 bilioni kila siku nayanayoongeza manunuzi ya nchi kutoka nje (imports) na hivyokupoteza
fedha za kigeni hovyo.
Mheshimiwa
Spika, Wizara
ya Fedha ambayo ndio wizara mama yaPPRA kupitia Fungu 50, na ndio Wizara yenye
kusimamia uchumi wanchi kwa ujumla ituletee Bungeni Taarifa ya
Uchunguziutakaofanywa na PPRA kuhusu manunuzi shilingi 1.4 bilioni kila sikuya
mafuta kuendesha mitambo ya kuzalisha Umeme.
2.3 Deni
la Taifa.
Mheshimiwa
Spika, Fungu
22 linaombewa jumla ya shilingi bilioni2,735 ili kuweza kulipa madeni ikiwemo deni
la nje la shilingi bilioni373 na trilioni 1.5 kama deni la ndani. Kwa mujibu wa
taarifa yamwenendo wa uchumi ya mwezi Julai 2012, deni la nje la Taifa(external
debt) mpaka mwisho wa mwezi Juni 2012 lilikuwa limefikiakiasi cha dola za
Kimarekani milioni 10,354.6 kiasi ambacho niongezeko la zaidi ya dola milioni
385.9 kwa
kipindi kama hichomwaka 2011. Aidha katika kipindi hicho deni la ndani lilikuwa
kiasicha shilingi bilioni
4,174.2 .
Kambi ya Upinzani Bungeni ina taarifakwamba takwimu hizi za Deni la Taifa
hazihusishi dhamana ambazoSerikali imezitoa kwa Mashirika ya Umma na Kampuni
binafsi.Dhamana lazima katika siku za usoni ziwe ni sehemu ya deni la
Taifamaana tumeshuhudia sasa ambapo Kampuni nyingi binafsizimeshindwa kulipa
mikopo iliyodhaminiwa na Serikali. Mfano nimalipo ya deni lenye thamani ya
shilingi bilioni 60 la kukodishandege ya Airbus kwa Shirika la ATCL kutoka
kampuni ya WallisTraders ya Lebanon na Deni lililochukuliwa na Kampuni ya
KiwiraCoal and Power limited ambayo mbia wake alishindwa kuendeshamradi wa
Makaa ya Mawe Kiwira licha ya kudhaminiwa na SerikaliMkopo kutoka kwenye
taasisi za Fedha hapa nchini ambapo sasaSerikali imepanga kulipa shilingi
bilioni 40 katika Bajeti ya mwakahuu.
Mheshimiwa
Spika, Kambi
Rasmi ya Upinzani haina tatizo nauhimilivu wa Deni la Taifa (Debt
sustainability) kwani tunajua kuwamataifa makubwa yanakopa sana na yana uwiano
mkubwa waDeni kwa GDP kuliko sisi. Tatizo letu ni namna ambavyo fedha zamikopo
zinatumika. Matumizi ya mikopo tunayochukua sio endelevumaana sehemu ya mikopo
hiyo hutumika kwa matumizi ya kawaidabadala ya matumizi ya uzalishaji au
kuongeza uwezo wetu wakuzalisha.
Kambi
Rasmi ya Upinzani inaendeleza
wito wake wa kutaka Fungu22 la deni la Taifa lifanyiwe ukaguzi maalum (Special
Audit) ili tuwezekujua mikopo hii tunayochukua kila wakati inatumika kufanyia
nini?Miradi iliyotekelezwa kutokana na Madeni ambayo Waziri wa Fedhaaliitangaza
wakati wa kufunga mjadala wa Bajeti kuu ya Serikaliifanyiwe ukaguzi kutambua
ukweli na kuona thamani ya Fedha.
Mheshimiwa
Spika, Kambi
Rasmi ya Upinzani inaendelea kuhojikama tulivyohoji mwaka 2011/2012 kuhusu
matumizi mabaya yafedha za umma. Katika fungu 21, kasma 229929, Serikali
imetengaShilingi bilioni 26.4 kwa ajili ya kulipa fidia kwa mikataba
mbalimbaliambayo Serikali imeingia. Hii inaonyesha kuwa Serikali inatumiafedha
nyingi sana kwa ajili ya mikataba iliyoingiwa na Mashirika yaUmma na kuliletea
hasara Taifa.
Mheshimiwa
Spika, Kambi
Rasmi ya Upinzani pamoja na kutakamajibu kutoka kwa serikali, bado tunataka
kuwe na usimamizi thabiti ili kulinda fedha za umma zinazotumika kwenye
Mashirika ya Umma,ambapo kumekuwa na usimamizi mbovu sana na unaopelekeaTaifa
kupoteza fedha nyingi sana kutokana na ubadhirifu katikaMashirika ya Umma. Hii
ni kweli kwa Mashirika ambayo Serikaliinamiliki sehemu ya hisa.
2.5 MKOPO
WA KUNUNUA RADA ILIYOGUBIKWA NA UFISADI
Mheshimiwa
Spika, sehemu ya
Malipo ya Deni la Taifa ni Mkopoambao Serikali ilichukua ili kununua Rada
kutoka kampuni ya BAE yaUingereza. Suala hili la rada limejadiliwa sana nchini
kwa upandemmoja tu wa ufisadi wa kupandisha bei ya Rada na hatimayekurejeshwa
kwa iliyoitwa chenji ya Rada. Hiyo ilikuwa ni nusu tu yaukweli kuhusu suala la
Rada kwani Serikali ilikopa kiasi cha dola zakimarekani 40 milioni kutoka Benki
ya Barclays ya Uingereza kwa ajiliya kununulia Rada. Mkopo huo ulikuwa na Riba
ya asilimia 4.9 juu yakiwango cha riba zinazotolewa na Benki ya Dunia au IMF.
Kambi
Rasmi ya Upinzani inataka
kujua kama mkopo huuumeshalipwa wote na jumla tulilipa kiasi gani cha fedha.Ukilinganisha
fedha iliyorejeshwa kama chenji ya Rada na Fedhaambayo Tanzania iliilipa Benki
ya Barclays (Principal amount naInterest), je chenji ya Rada ilikuwa na thamani
yoyote kifedha?Mjadala wa ununuzi wa Rada hauwezi kuisha kwa
kufurahiakurejeshewa chenji tu. Mjadala huu bado mbichi kabisa kwanitunataka
ukweli na ukweli mtupu uelezwe kwa umma na kuona Taifa lilipata hasara kiasi
gani kwa ufisadi huu wa kimataifa na hatuastahiki za kisheria kuchukuliwa dhidi
ya wote walioingiza hasara kwaTaifa letu.
2.4 Kitengo
cha Udhibiti wa Fedha Haramu
Mheshimiwa
Spika, taifa
letu limekuwa na sheria nyingi ambazoziliwahi kutungwa kwa ajili ya kukabiliana
na tatizo la fedha haramu,rushwa na uhalifu uliopangwa hapa nchini mwetu tangu
tupateuhuru na hii inathibitishwa na uwepo wa sheria zaidi ya 15 kuwahikutungwa
tangu uhuru (tazama kiambatanisho A ). Vile vile Bungeliliimarisha Sheria ya
Udhibiti wa Fedha Haramu mwaka 2011. Hatahivyo bado nchi yetu imegubikwa na
fedha chafu na hasa wizikatika Mabenki hapa nchini. Wakati sheria ya Fedha
haramuinayataka Mabenki kutunza kumbukumbu sahihi za wateja,kumekuwa na matukio
(yaliyoripotiwa na yasiyoripotiwa) yaWafanyakazi wa mabenki hapa nchini
kushirikiana na baadhi yawananchi kuiba fedha za wateja na hasa wateja
ambaowamefariki dunia na ndugu na jamaa zao kutojua taarifa za kibenkiza
marehemu hawa. Serikali inapaswa kufahamu kuwa wizi kwenyemabenki ni moja ya
sifa mbaya sana ya mfumo wetu wa fedha nahivyo kusababisha Benki kuweka riba
kubwa sana ili kufidia ‘risk’kama hizi za watu ‘kupiga’ amana za wateja kwenye
mabenki. Kambi Rasmi ya upinzani inaitaka Wizara ya Fedha kupitia Kitengo cha
Udhibiti wa Fedha haramu kudhibiti wizi kwenye Benki za hapanchini.
Mheshimiwa
Spika, Kambi
Rasmi ya Upinzani inataka kupatamaelezo ya kina juu ya matatizo ya mtaji “
Capital under pressure” yanayoikabili benki ya NBC na hatua
zilizochukuliwa na Serikali kamammoja wa wanahisa dhidi ya mwanahisa mwenye
dhamana yakuisimamia Benki hiyo (ABSA) kwa kushindwa kuisimamia kwaumakini na
hivyo kuiingiza katika matatizo hayo ya mtaji.Mheshimiwa Spika, hivi sasa
wanahisa (ambapo Serikali ni mmojawao) wanapaswa kuongeza mtaji katika benki ya
NBC ili kuinusuru,Benki ambayo ni moja ya Benki kubwa kabisa hapa nchini
ambayokama ingekuwa na usimamizi mzuri ingepaswa kujiendeshayenyewe na kutoa
gawio kwa wanahisa.
Mheshimiwa
Spika, taarifa
iliyotolewa na Benki Kuu ya Uswissi nakuchapishwa na magazeti mbalimbali ya
hapa nchini mwezi June,2012 inanonyesha kuwa viongozi wa Serikali pamoja
nawafanyabiashara wakubwa wametorosha fedha zao katikamabenki ya Uswissi kiasi
cha shilingi bilioni 315.5. Habari zaidizinaeleza kwa mba mabilioni haya
yanatokana na ‘deals’ zilizofanywa na watendaji wa Serikali na wafanyabiashara
kadhaakwenye sekta za Nishati na Madini. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeniimepata
taarifa kuwa mmoja wa Viongozi wa juu kabisa wa Tanzania na baadhi ya Mawaziri
wa Serikali za awamu zilizopita nimiongoni mwa wamiliki wa Fedha hizi. Sehemu
kubwa ya Fedhazililipwa na Kampuni za utafutaji wa Mafuta na Gesi katika Pwani
yaMkoa wa Mtwara zilizopewa mikataba kati ya mwaka 2004 na 2006.Kambi Rasmi ya
Upinzani inaitaka Serikali kutoa taarifa rasmi yahatua gani imechukua mara
baada ya taarifa ile kutoka Benki yaTaifa ya Uswissi ilipotolewa.
Tunaitaka
Serikali kuliambia Taifa hatuaitakazochukua kurejesha fedha hizi na nyingine
zozote ambazozimefichwa ughaibuni. Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni
italazimikakuweka wazi taarifa na majina ya watu wenye umiliki wa fedhakatika
Benki za nchini Uswissi iwapo Serikali haitatoa taarifa rasmikuhusu suala hili.
Mheshimiwa
Spika, Aidha,
kuna taarifa nyingine zinaonyesha jinsiambavyo taifa linaibiwa kupitia kesi
mbalimbali ambazo Serikaliimeshitaki au kushitakiwa kwenye Mahakama za
Kimataifa. Mfanomzuri ni Kesi ya IPTL na Standard Chartered Bank ya Hong
Kongambayo imechukua muda mrefu bila kuisha na kuliingizia taifahasara kubwa
sana. Tunapenda kufahamu ni kwa nini mpango wakumaliza kesi hii nje ya Mahakama
hautekelezwi na vile vile mpangowa kugeuza Mtambo wa kufua umeme wa IPTL kuwa
wa Gesi kwanini hautekelezwi?
Kambi
Rasmi ya Upinzani inataka
kupata majibu kuhusu mamboyafuatayo; Kwanza, fedha zilizoko kwenye Escrow
Akaunti Benki Kuu za IPTL(Tegeta escrow) zimefikia kiasi gani mpaka sasa, na
usalama wafedha hizo ukoje? Ikumbukwe kwamba kuna uamuzi wa Bungekwamba Fedha
hizi zisitumike wala kutolewa mpaka maamuzikuhusu mtambo wa IPTL kufikiwa na
hasa uamuzi wa kugeuzamtambo huu kutumia Gesi Asilia.Pili, Suala hili la kesi
ya IPTL limechukua muda mrefu sana na sasa niwakati muafaka likamalizwa nje ya
mahakama kwa Waziri waFedha kukutana na pande zote za mgogoro huu ili liweze
kufikiamwisho.
2.6
Kampuni ya Oxford University Press Tanzania KufungiwaMheshimiwa Spika, mnamo
tarehe 03 Julai 2012 Benki ya Duniailitangaza kuifungia kampuni ya uchapishaji
ya Oxford UniversityPress Tanzania Ltd (OUPTL) kutokana na vitendo vya
rushwaambavyo kampuni hiyo ilikiri kuhusika kwake kwenye miradimbalimbali ya
elimu iliyokuwa inafadhiliwa na Benki hiyo katikaukanda wa Afrika Mashariki.
Mheshimiwa
Spika, kampuni
hiyo ilikiri kuhusika katika kuwahongamaafisa mbalimbali wa Serikali katika
mkataba wake wakusambaza vitabu na kampuni hiyo ilikubali kuilipa Benki ya
Duniakiasi cha dola 500,000 kama sehemu ya makubaliano yakekutokana na kashfa
hiyo.
Mheshimiwa
Spika, mamlaka
ya manunuzi ya umma ilitangazakuifungia kampuni hiyo hapa nchini kwa kipindi
cha miaka saba,wakati ambao tayari tulishawapa zabuni ya kusambaza
vitabuvilivyotokana na chenji ya rushwa ya Rada ambazo ziliamuliwakuwa zitaenda
kununua vitabu.
Kambi
Rasmi ya Upinzani inaitaka
Serikali kuinyang ’anya kampunihii zabuni ya kuchapisha na kusambaza vitabu
hivyo na badalayake kazi hiyo yapewe makampuni ya ndani ya nchi. Tabia
yaSerikali kufanya kazi na Kampuni ambazo tayari zina dosari ama zakifisadi au
kukiuka sheria na maagizo ya Serikali inatoa picha mbayakwenye uchumi. Hali
kadhalika, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitakaSerikali kuwachukulia hatua maafisa
wote wa Wizara waliohusika katika “rushwa ya Oxford”.
3.0
Mishahara hewa nchini
Mheshimiwa
Spika, katika
hotuba ya Msemaji Mkuu wa Kambi Rasmiya Upinzani kuhusu makadirio ya mapato na
matumizi katika Ofisi yaRais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma kwa mwaka wa
fedha2012/2013, tulitaja kiasi cha shilingi bilioni 9 1 ambazo zililipwa
kamamishahara kwa watumishi hewa kama ilivyoripotiwa na magazeti ya The Daily
News’ na ‘The Guardian ’ya Machi 23, 2011.
Mheshimiwa
Spika, ripoti ya
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabuza Serikali ya tarehe 31 Machi, 2012
inaonesha kwamba kwa mwakawa fedha 2010/2011 jumla ya shilingi 142,715,827.992 zililipwa
kamamishahara kwa wastaafu, watumishi walioacha au kufukuzwa kazina watumishi
wengine ambao hawakustahili. Aidha, ripoti hiyoimeonesha kiasi cha shilingi
1,842,607,565.29 zilizolipwa kamamishahara hewa kwa mwaka wa fedha 2009/2010.
Mheshimiwa
Spika, kwa
mujibu wa taarifa ya Waziri wa Fedha kwakamati ya kudumu ya Bunge ya fedha na
uchumi ya tarehe 7Agosti, 2012 ni kwamba uhakiki wa watumishi uliofanyika
mweziJanuari, 2012 kwenye Halimashauri 133 na kwenye taasisi na wakalaza
Serikali 154 ulibaini majina 9,949 ya watumishi wasiostahili kuwemokwenye
orodha ya mishahara. Idadi hii ya watumishi hewa nisawasawa na takribani idadi
ya watumishi walioajiriwa katika sektanzima ya madini kwenye migodi ya dhahabu
hapa nchini.Watumishi hewa wanaokaribia 10,000 ni wengi mno na
inaonyeshadhahiri namna Serikali isivyo makini katika suala hili
ambalolinasababisha upotevu mkubwa wa Fedha za Umma.
Mheshimiwa
Spika, Waziri wa
Fedha alikiri mbele ya Kamati yaFedha na Uchumi kwamba mwezi Februari Serikali
ililipa shilingi bilioni5.1 kama mishahara hewa. Hii maana yake ni kwamba
Serikali. hutumia zaidi ya shilingi bilioni 70 kila mwaka kwa watumishi hewawa
Serikali.
Mheshimiwa
Spika, tunataka
fedha hizi wanazolipwa watumishihewa zitumike kuwalipa walimu na madaktari
madai yao kwani ninyingi na zinatosha sana. Siku zote sababu za Serikali
kutotimizamatakwa ya wafanyakazi kwenye sekta ya Afya na Elimu nikwamba
Serikali haina Fedha. Lakini hapa tunashuhudia Shilingibilioni 70 kila mwaka
zikiteketea kulipa watumishi hewa ambaohawapo, hawafanyi kazi na hivyo
kufaidisha mtandao wa kifisadiambao kwa vyovyote vile unaanzia Wizara ya Fedha
na Wizara yaUtumishi. Serikali inakosa vipi fedha za kulipa madai ya Walimu
nainapata za kulipa watumishi hewa? Serikali inakosa vipi fedha zakulipa
Madaktari na Manesi lakini inapata shilingi bilioni 70 kilamwaka kulipa
watumishi hewa?
Mheshimiwa
Spika, Kambi
Rasmi ya Upinzani inataka mradi huu wawatumishi hewa wenye mauzo (turnover) ya
shilingi 70 bilioni kwamwaka uvunjwevunjwe ili kupata fedha za kulipa Walimu
naMadaktari. Waziri wa Fedha asambaratishe mtandao huu mwovuambao sasa umeota
mizizi kwenye Taasisi za Serikali. Vile vile Waziriagawe kwa Wabunge taarifa ya
uhakiki wa wafanyakazi wa Serikalina pia hatua ambazo Serikali imechukua dhidi
ya vinara wamtandao wa watumishi hewa Serikalini.
4.0 Benki
Kuu ya Tanzania-(BOT)
Mheshimiwa
Spika, taasisi
hii ndiyo yenye dhamana ya kutayarishana kusimamia sera za fedha na utendaji
mzima wa taasisi za fedhakwa ujumla. Katika kutekeleza hilo Benki Kuu ndicho
chombokinachoweka miongozo kwa taasisi za fedha, taasisi za bima nataasisi za
hifadhi za jamii ili kuhakikisha fedha za wanachama katikataasisi hizo
zinalindwa.
Mheshimiwa
Spika, taasisi
za fedha zimegawanyika katika sehemukuu mbili, ambazo ni tasnia ya benki (Banking
industry ) na tasniandogo ya fedha (Microfinance industry). Tasnia zote
hizizinahudumia wateja tofauti kwa kulingana na wanachojishughulishanacho
katika kuinua kipato cha familia inayomtegemea, mteja yukokwenye sekta binafsi
au sekta rasmi ya ajira.
Mheshimiwa
Spika, Benki
Kuu katika kutimiza wajibu wake inailazimukutoa vigezo vitakavyozingatiwa
katika utoaji wa mikopo ilikukabiliana na wakopaji ambao wanaweza kuwa na lengo
lakuchukua fedha wakati hawana nia ya dhati ya kurejesha mikopoyao.
4.1 RIBA
KATIKA TAASISI ZA FEDHA
Mheshimiwa
Spika, tofauti
kati ya viwango vya riba vinavyotozwakwenye mikopo na vile vinavyotolewa kwenye
amana kama faidavimeendelea kuwa juu, licha ya kuongezeka kwa ushindani
katikasekta ya kibenki. Hii imechangiwa kwa kiasi kikubwa na kukosekanakwa
taarifa sahihi za wakopaji (credit reference data bank) na kutokuwepo kwa
taasisi ya utoaji wa taarifa sahihi za waombajimikopo (Credit Rerefence Bureau)
nchini. Aidha, gharama kubwaza kufanya biashara kutokana na miundombinu hafifu,
nazozimechangia kuongeza viwango vya riba vinavyotozwa kwenyemikopo. Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni inaomba taarifa yakuanzishwa kwa Credit Reference
Bureaux kwa mujibu wa Sheria yaBenki na Taasisi za Fedha ya mwaka 2006.
4.2
Usimamizi Wa Tasnia Ndogo ya Fedha (Microfinance Industry-MFI)
Mheshimiwa
Spika,tasnia
hii ndiyo inayoshughulika moja kwa mojana kundi kubwa la Watanzania ambao
hawako kwenye mfumorasmi wa ajira kwa kuwapa mikopo midogo midogo kwa
shughulirasmi au zisizo rasmi, ili kuhakikisha kuwa kipato cha familiakinapanda
na hivyo uchumi wa mwananchi mmoja mmoja unakua.
Mheshimiwa
Spika, tasnia
hii inalenga kuboresha maisha yawananchi wa vijijini na maeneo mbalimbali ya
mijini. Tasnia hiiinalenga kuboresha maisha kwa wananchi mmoja mmoja aumakundi
(Saccoss) na benki jamii (vicoba) ambazo zimekuwa nawanachama wengi
wanaoendelea kujiunga ili kujikwamuakiuchumi.
Mheshimiwa
Spika,
kukosekana kwa mdhibiti anayeelewa jinsi tasniahii inavyofanya kazi zake na
aina ya wateja inaowahudumia ni udhaifu mkubwa unaosababisha tasnia hii
kushindwa kukua.Kukosekana kwa udhibiti wa sekta ndogo ya Fedha
kunasababishawananchi masikini kuumia sana. Mfano tumeshuhudia namnaKampuni za
kukopesha zinavyowafanya Walimu vijijini kuwa masikinizaidi kwa kuweka riba
kubwa sana. Hata hivyo Serikali imekaa kimyabila kusaidia wanyonge hawa kwa
kuchukua hatua madhubuti zakudhibiti na kusimamia sekta hii. Mfano mzuri wa
Serikali kushindwakusaidia wanyonge ni pale ambapo wannachi wengi sana kujikuta
wamepoteza fedha zao kupitia ‘schemes’ kama vile DECI ambapo wananchi
walikusanya zaidi ya shilingi bilioni 16 ambazo mpaka sasahata riba yake
hatujui inakwenda wapi? Kungekuwa na Mamlakaya kusimamia sekta ya fedha kwa
ajili ya wanyonge tusingeshuhudiaunyonyaji huu.
Mheshimiwa
Spika, Kambi
Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuundaMamlaka ya Usimamizi wa sekta ndogo
ya Fedha (TanzaniaMicrofinace Regulatory Authority) hapa nchini badala ya Benki
Kuuya Tanzania ambayo ndiyo msimamizi wa tasnia ya benki. Lengo nikuhakikisha
kuwa wananchi wa vijijini wanaopata mikopo kutokakwenye taasisi za Benki
wanalindwa na dola. Mamlaka italinda Haki za wanyonge dhidi ya ‘loan sharks’ na
Wajibu wa wanyonge wenye kuchukua mikopo.
Mheshimiwa
Spika, kuundwa
kwa chombo chenye mamlaka yakusimamia taasisi ndogo ya fedha ni lazima kutokana
na ukweli kwamba kuna utofauti wa muundo baina ya mabenki na taasisindogondogo
za fedha; inakuwa ni vigumu kudhibiti riba na utoajiwavigezo vya kifedha katika kuhudumia wananchi na kutoamikopo kwa wateja wa
tasnia hizo mbili zilizo tofauti kimuundo.
Mheshimiwa
Spika, kuwepo
kwa chombo chenye mamlaka piaitasaidia kuwa na Credit Reference Bureau
itakalokuwa na taarifaza wakopaji kutoka taasisi ndogondogo za fedha tofauti
naitakayosimamia wadaiwa wa mabenki na taarifa hizi zitasaidiaudhibiti wa
wateja wa taasisi hizi kuchukua zaidi ya mkopo mmojakwenye taasisi tofauti
tofauti ambapo hali hii husababishwa naucheleweshaji wa mikopo inayotolewa na
taasisi hizi pamoja nauhafifu wa mikopo katika kumsaidia mlengwa.
4.3
Mifuko ya Hifadhi za Jamii
Mheshimiwa
Spika,Mifuko ya
Hifadhi za Jamii ni mojawapo ya sektaambayo ina uwezo mkubwa wa kupunguza
ukosefu wa ajira kwavijana wetu, kama uwekezaji unaofanywa kwa kutumia mifuko
hiyoutasimamiwa vizuri.
Meshimiwa
Spika, inaonesha kwamba mifuko hii imekuwa
ikikusanyamichango ya wanachama na kulipa wastaafu wanachama waMifuko hii
vizuri. Kutokana na maelekezo ya sheria mpya iliyoletamjadala baina ya
wafanyakazi na serikali juu ya mabadiliko yasheria na utoaji wa mafao kwa
wafanyakazi, pamoja na Bungekutaka mabadiliko ya sheria hiyo bado kuna haja ya
kutazamanamna mifuko ifanyavyo kazi.
Kambi
Rasmi ya Upinzani inaitaka
serikali kuweka wazi utendaji waMifuko hii katika maeneo nyeti yafuatayo,
kwanza Ukwasi wake (Liquidity of the Social Security funds), pili Uwekezaji
(Investments) piaRisk Management reports. Taarifa katika maeneo haya
hupelekwana mifuko kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika yaUmma na
kutokana na utaratibu wa Kazi wa Kamati hii ya POAC nivigumu wananchi wote
kuona taarifa hizi ambazo ni muhimu kuwawazi kwa umma. Taarifa kama hizi
zitaliwezesha Bunge kuelewakiwango cha usalama wa Mifuko hii na uwezo ziada
(excessfinancial capacity) kuendelea kutoa huduma zinazohitajika. Kamailivyo
kwa Mabenki, tunashauri kuwa taarifa za robo mwaka zaMifuko ya Hifadhi ya Jamii
ziwe zinatangazwa kwenye magazetiyanayosomwa zaidi nchini ili wananchi na hasa
wanachama wamifuko waone namna mifuko yao inavyofanya kazi.
Mheshimiwa
Spika, aidha,
kwa kuwa Kambi Rasmi ya Upinzani kwakipindi chote imekuwa ikitoa ushauri katika
sekta hii, hatuna budikurudia ushauri tulioutoa mwaka jana kama ifuatavyo: “
Mheshimiwa
Spika, Kambi ya
Upinzani inapendekeza kwa Mifukoya PSPF na PPF kuangalia namna ya kuwekeza
katika maeneoyanayochochea ukuaji wa uchumi na hivyo kuzalisha ajira na kupata
wanachama zaidi. Maeneo kama uwekezaji kwenyeBandari na Reli yanapaswa
kuangaliwa kwani kutokana na Jiografiaya nchi yetu ni maeneo yanayoweza
kuzalisha faida kubwa sana.Tunaitaka Serikali ilieleze Bunge kuna mipango gani
katika Mashirikahaya (PSPF na PPF) kuangalia maeneo mapya ya uwekezaji
katikamiundombinu na hasa Bandari.
Mheshimiwa
Spika, Mifuko ya
hifadhi ya jamii imewekeza katikamiradi ya ujenzi wa nyumba nafuu kwa ajili ya
wanachama wao napia wanachi kwa ujumla. Tunasisitiza Miradi hii isiwe Dar es
salaamna Mwanza tu bali ienee nchi nzima kama ambavyo mfuko wa PSPFumeanza.
Mheshimiwa
Spika, Kambi ya
Upinzani pia inashauri kwamba fao laElimu ambalo Mfuko wa PPF unatoa kwanza
litolewe na Mifukomingine pia lakini pia lipanuliwe hadi kufikia elimu ya Chuo
Kikuu.Fao hili la Elimu ambalo ni muhimu sana na twapongeza mfuko waPPF kwa
kulianzisha ni fao ambalo litasaidia sana kuhakikisha kuwayatima ambao wazazi
wao wanakuwa wamefariki wanapatauhakika wa kuendelea na masomo. Fao hili liwe
fao la lazima kwamifuko yote nchini.
Mheshimiwa
Spika, Kambi ya
Upinzani Bungeni bado inasisitizaushauri wake kuwa
Mifuko
yote ya Hifadhi ya Jamii ihamishiweWizara ya Kazi na Ajira kama Wizara inayo husika
na ‘social security’. Hoja hii inatiliwa nguvu na uhalisia kwamba Mdhibiti wa
Mifuko (SSRA) yupo chini ya Wizara ya Kazi. Vile vile Wizara ya Fedha
kamamlipaji mkuu wa Pensheni asiwe na Taasisi hata moja ya Pensheni chini yake
ili kuweka ‘checks’.
Mheshimiwa
Spika, Hali
kadhalika hakuna sababu ya kuwa na utitiriwa mifuko mingi kama ilivyo sasa.
Ipunguzwe na kubakia na mifukomiwili tu, mmoja wa wafanyakazi walio katika
sekta binafsi na sektaisiyo rasmi na mwingine kwa wafanyakazi wa sekta ya umma
.Tunarejea pendekezo letu kwamba mifuko ya NSSF na PPFiunganishwe kuwa mfuko
mmoja kwa ajili ya sekta binafsi na sektaisiyo rasmi na mifuko ya PSPF, LAPF na
GEPF iunganishwe kuwamfuko mmoja kwa ajili ya kushughulika na wafanyakazi wa
Sekta yaUmma”.
Mheshimiwa
Spika,
mojawapo ya vipaumbele vya Kambi Rasmi yaUpinzani kwa mwaka 2012/2013 ni
kupunguza misamaha ya kodi yakutozidi asilimia moja ya GDP, kutokana na Mapato
mengi ya Serikalikupotea kwa sababu ya kutoa misamaha ya kodi kwa
wadaumbalimbali wanaotakiwa kulipa kodi, na ikizingatiwa moja yamichango ya
waziri akiwa mbunge tarehe 25/8/2011 alisema “kupunguza misamaha ya kodi ya
kutozidi asilimia moja ya GDP”.Kambi Rasmi ya Upinzani inaamini waziri alikuwa
na nia ya dhati nakukubaliana na Kambi Rasmi ya Upinzani uwezekano wa jambo
hili.Hivyo basi, ili kuonesha kuwepo kwa dhamira ya kweli Kambi Rasmi ya
Upinzani inataka waziri alijulishe bunge juu ya utekelezaji waazimio hili.
6.0
MSAJILI WA HAZINA NA BODI ZA MASHIRIKA YA UMMA.
Mheshimiwa
Spika, itakumbukwa
kuwa mnamo mwaka 2010 Sherianamba 2 (the written laws (miscellaneous
amendments) No 2. ACT2010 ilipitishwa na katika eneo la kumi (part X) ilifanyia
marekebishosheria ya mashirika ya umma (the public Corporations Act, CAP257).
Sheria hii ilisainiwa na Rais mnamo tarehe 20 Mei 2010.
Mheshimiwa
Spika, katika
mabadiliko hayo ya sheria ibara ya 20 na21 ilibainisha bayana majukumu ya
msajili wa hazina na ndipoiliweka majukumu yake ya kazi kuwa ni kusimamia
mashirika yote yaumma. Aidha, mabadiliko hayo yalibainisha wazi kuwa msajili
wahazina hatakuwa mjumbe wa Bodi za mashirika haya na walahapaswi kushiriki
kwenye vikao vya bodi vya mashirika haya kwaniyeye ni msimamizi mkuu wa
mashirika hayo na anapaswa kusimamiautendaji kazi wake.
Mheshimiwa
Spika, pamoja
na mabadiliko hayo ya sheria badomsajili wa hazina amekuwa akihudhuria vikao
mbalimbali vya bodiza Mashirika ya Umma kama mjumbe jambo ambalo ni kinyume
nasheria, na amekuwa akishiriki moja kwa moja kwenye maamuzi yabodi hizo jambo
ambalo linamfanya kushindwa kutimiza wajibuwake wa kuwa msimamizi kama ambavyo
sheria inaelekeza.
Kambi ya
Upinzani inataka
kupata maelezo ya kina ni kwa nini halihii imeendelea kuachwa iwe ilivyo kwa
msajili wa hazina kuendeleakuwa mjumbe wa vikao vya Bodi za mashirika ya umma
kinyume nasheria. Aidha tunataka kauli ya serikali kuhusiana na suala hili.
Mheshimiwa
Spika, Kambi ya
Upinzani inapenda kupata maelezo yaSerikali kuhusu masuala yafuatayo.Moja,
Sakata la uuzwaji wa hisa za Shirika la UDA umefikia wapi?Pili, Serikali
imefikia wapi katika utungaji wa Sheria mpya ya Ofisi yaMsajili wa Hazina ili
kuimarisha usimamizi wa Mashirika ya Umma.Tatu, Serikali imefikia wapi katika
pendekezo la kuifanyiamarekebisho Shirika Hodhi la Mashirika ya Umma (CHC) ili
liwezekumiliki, kusimamia na kuziendesha hisa za serikali katika Kampunibinafsi
ambapo umiliki wa Serikali ni chini ya asilimia 50. Pendekezohili lilikuwa ni
uamuzi wa Bunge na hivi sasa mwaka mzima umepitabila Bunge kupatiwa taarifa
yeyote kinyume na maelekezo yake.Nne, Serikali imefikia wapi katika utekelezaji
wa Waraka nambamoja wa mwaka 2012 kuhusu usimamizi na uendeshaji wa Mashirikaya
Umma na hasa mahusiano kati ya Mashirika ya Umma na Wizaramama. Waziri wa Fedha
kama msimamizi mkuu wa Mashirika ya Umma amechukua hatua gani kuhakikisha falsafa
ya ‘eyes on,hands off’ katika kusimamia Mashirika ya Umma inatekelezwa
kikamilifu na kuhakikisha Mashirika ya Umma yanaendeshwa kwafaida na bila
kuingiliwa ingiliwa na Wanasiasa?
7.0 Ofisi
ya Takwimu ya Taifa
Mheshimiwa
Spika, Ofisi
ya Taifa ya Takwimu (National Bureau ofStatistics NBS) ilizinduliwa rasmi
tarehe 26 Machi, 1999 kamaWakala wa Serikali (Executive Agency) kwa mujibu wa
Sheria yaWakala wa Serikali Na. 30 ya mwaka 1997, (The Executive AgenciesAct
1997) (Act No. 30 of 1997), na ndio chombo rasmikinachojihusisha na kutafuta,
kuandaa na kusambaza takwimuhapa Tanzania.
Mheshimiwa
Spika, katika
kupanga mipango ya maendeleo nakuandaa sera mbalimbali za nchi husika,
upatikanaji wa takwimurasmi zinazotokana na Kanuni na Mbinu za Kitaalamu
iliyowekwa naOfisi ya Takwimu ya Umoja wa Mataifa (United Nations
StatisticalDivision) ni muhimu. Takwimu zote zilizo rasmi duniani hutolewa
naOfisi za Takwimu za nchi husika kupitia Sheria za Takwimu za nchimbali mbali.
Mheshimiwa
Spika, Kambi
Rasmi ya Upinzani imekua ikitoaMapendekezo ya kuboresha utendaji wa Ofisi ya
Takwimu katikaNyanja mbalimbali na serikali kutothubutu kuchukua
mapendekezohayo na kuyafanyia kazi.
Mheshimiwa
Spika, katika
taarifa ya miaka hamsini ya wizara,taarifainaonesha wizara kuwa na nia ya
kuboresha ofisi ya takwimu yataifa kwa kuboresha miundombinu ya utoaji takwimu
nchini,kuimarisha mfumo wa takwimu nchini (NBS), kutoa takwimu sahihina kwa
wakati, kutokana na nia hii ya serikali Kambi Rasmi yaUpinzani inaitaka
serikali kuzingatia Ofisi ya Takwimu Kuwa nauhisiano wa moja kwa moja wa Ofisi
ya Takwimu ya Taifa na ngaziza Mikoa, Halmashauri za Wilaya, Kata na Vijiji
kurahisisha upatikanajiwa takwimu ili zisaidie katika kupanga mipango ya
maendeleo.
8.0
Mamlaka Ya Mapato-TRA
Mheshimiwa
Spika, Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni inapendekezakwamba Mamlaka ya Mapato Tanzania ijenge
uwezo wa kukaguamahesabu ya kikodi kwenye Kampuni za Utafutaji wa Mafuta
naGesi, Kampuni za Madini na Kampuni za Simu ambazo uzoefuunaonyesha kuwa
katika maeneo haya kuna mbinu nyingi sana zakukwepa kodi.
Mheshimiwa
Spika, kwa
msisitizo mkubwa sana Kambi Rasmi yaUpinzani Bungeni inaitaka mamlaka ya Mapato
Tanzaniakushirikiana kwa karibu na Mamlaka ya Mawasiliano nchini kukaguamapato
ya Kampuni za simu na hasa kampuni ambazo zinatoahuduma kwenye kampuni za Simu.
Mheshimiwa
Spika, Katika
mjadala wa Bajeti ya Wizara yaMawasiliano kulikuwa na mjadala kuhusu namna
ambavyo wasaniiwa Tanzania wanavyonyonywa mapato na Kampuni zinazotoahuduma ya
miito kwenye kampuni za simu. Bunge lako lilielezwakwamba Biashara ya miito
kwenye simu ina thamani ya shilingi bilioni43 kwa mwaka lakini msanii
anayetengeneza kazi zinazouzwaanapata asilimia 7 tu ya mapato hayo.
Mheshimiwa
Spika, taarifa
zaidi za ziada zinaonyesha kuwa kampuniya On Mobile yenye mkataba na Kampuni za
Simu za Vodacom na Airtel kama ‘aggrigator’ wa miito ya simu yenye miziki ya
wasaniihapa nchini hailipi kodi kutokana na mapato yake. Kambi Rasmi yaUpinzani
inaitaka Serikali kutoa taarifa za kikodi za kampuni hii nawashirika wake na
hatua ambazo Serikali imechukua dhidi yao.Kambi ya upinzani inashauri pia
kwamba Mapato yanayotokana na miradi kama hii kwenye Kampuni za simu yawe ‘ring
fenced’ na kutozwa kodi stahiki au kodi maalumu.
9.0 Ofisi
ya Mkaguzi Mkuu wa Ndani-Internal Auditor General
Mheshimiwa
Spika, Ofisi
ya Mkuguzi Mkuu wa Ndani (Internal Auditor General) iliyoanzishwa na
mabadiliko ya Sheria ya Fedha ya mwaka2010 inakabiliwa na changamoto mbalimbali
ambazo zimekuwazikileta migongano katika maeneo ya kiutendaji na uwajibikaji,sheria
haipo wazi juu ya upatikanaji wa mtaalam huyo kamainavyotakiwa na sheria na 8
ya utumishi wa umma, kwa mfanokutangazwa kwa nafasi hizo na waombaji kufanyiwa
usaili.
Mheshimiwa
Spika, pamoja
na utata wa uteuzi wa mkaguzi wandani kama sheria ya utumishi wa umma
inavyoelekeza mkaguzi wandani anasimamiwa na Katibu Mkuu Hazina (Paymaster
General) ambaye naye ni mkaguliwa- kwa hiyo kunakuwa na mgongano wakimaslahi
uhuru wa ofisi ya mkaguzi wa ndani inaweza kukosa uhuruKambi Rasmi ya Upinzani
inaishauri serikali katika ofisi ya Mkaguzi waNdani (Internal Auditor General
office) ingepaswa iwe na bodiambako maalumu wangekuwa wanaripoti ili kuweka
uhuruunaofaa.
Mheshimiwa
Spika,
wakaguzi wa ndani ni waajiriwa wa serikali nahufanya kazi zao za ukaguzi kwa
kipindi chote ambacho shughuli zaserikali zikifanyika, mfano; katika
halmashauri wakaguzi hutakiwakuwajibika kuanzia upokeaji wa fedha kutoka
hazina, hadi kutumikakwake, Kambi Rasmi ya Upinzani inahoji serikali nini
nafasi yawakaguzi wa ndani kama ubadhirifu wa fedha za ummaumeendelea kuwepo
kama ripoti za mkaguzi mkuu wa hesabu zaserikali zinavyothibisha?
Mheshimiwa
Spika, katika
ushughulikiaji wa matumizi mabovu yarasilimali za umma serikali imekuwa
legelege hasa pale taarifa zinapotolewa na wakaguzi wa ndani ambao hutoa
taarifa marakwa mara na seriakali kukaa kimya, Kambi Rasmi ya Upinzaniinaitaka
serikali kutambua umuhimu wa taarifa hizi za wakaguzi wandani na kuhakiki
inachukua hatua stahiki pasipo kusubiri taarifa zamkaguzi mkuu wa hesabu za
serikali ambazo ukaguzi wakehufanyika kwa kuchelewa zaidi.
10.0
Utekelezaji wa Bajeti kwa Mwaka wa Fedha 2011/2012 Pamojana Mpango wa Maendeleo
kwa Mwaka 2012/2013
Mheshimiwa
Spika, katika
bajeti ya Wizara ya Fedha mwaka2011/2012 fungu Namba 50wizara ilitenga shilingi
bilioni 659 kwaajili ya miradi ya maendeleo na fedha zilizotumika hadi kufikia
Juni2012 ni shilingi bilino 402.7 ambapo fedha za ndani zikiwa shilingibilioni
78.65 sawa na asilimia 11.9 ya bajeti ya maendeleo hivyokutegemea fedha za nje
katika kutekeleza miradi ya maendeleokwa asilimia 88.1. Kambi Rasmi ya
Upinzani, pamoja na Serilialikutokubali kutumia mapato ya ndani zaidi katika
kugharimia miradiya maendeleo, I azidi kushauri serikali kuwa na Makati wa
dhati wamuda mrefu wa kuachana na utaratibu wa kutegemea misaada yanje. Mkakati
huo ulenge kuiongezea mapato kwa kutumia mbinumbalimbali za kodi.
Mheshimiwa
Spika, katika
bajeti ya 2012/2013 serikali imetengashilingi bilioni 546.51 kwa ajili ya
kutekeleza miradi ya maendeleo ambayo ni pungufu kwa asilimia 18 ya bajeti ya
mwaka 2011/2012ambapo serikali ilitenga shilingi bilioni 659. Katika bajeti ya
2012/2013ni asilimia 19.3 tu ya fedha za ndani ndizo zimeelekezwa kwenyemiradi
ya maendeleo na asilimia 80.7 ya makadirio ni fedha za njeikiwa ni mikopo ya
kibiashara na misaada. Kambi Rasmi ya Upinzaniinahoji: ni maendeleo yapi ambayo
serikali inadhamiria kwakutenga fedha ya maendeleo ambayo ni pungufu kwa
asilimia 18ya bajeti ya mwaka jana?
HitimishoMheshimiwa
Spika, Kambi ya
Upinzani Bungeni inasisitiza umuhimuwa kuisimamia vema Wizara ya Fedha katika
kusimamia uchumi wanchi. Tuna imani kwamba Waziri wa Fedha ndugu William
Mgimwana Manaibu wake Mhe. Janeth Mbene na Mhe. Saada MkuyaSalum wataweza
kukabili changamoto tulizoainisha katika hotubayetu na kufanyia kazi
mapendekezo ambayo tumeyatoa. Tumeonadalili za Wizara hii na hasa Waziri na
Manaibu wake kusikiliza katikamasuala ya Kikodi hivyo, tuna imani kwamba
wataendelea kusikiliza.
Kambi
Rasmi ya Upinzani haitasita
kutoa ushirikiano kwa lengo lakuleta maendeleo katika nchi yetu. Hata hivyo,
tutakosoa kwanguvu zetu zote na kuchukua hatua za kiuwajibikaji dhidi ya
njamazozote za kudhoofisha maendeleo ya Taifa na watu wake. Siku zotetutasimama
upande wa wanyonge na kuwasemea wasio na sauti,Watanzania milioni 30 wanaoishi
vijijini na kwenye dimbwi laUmasikini (The Bottom 30M).
Mheshimiwa
Spika, baada ya kusema hayo kwa niaba ya KambiRasmi ya Upinzani naomba
kuwasilisha.
……………………………………
Kabwe
Zuberi Zitto (Mb)
Waziri
Kivuli-Wizara ya Fedha
12.08.2012
KIAMBATANISHO
A.
Sheria
mbalimbali kuhusiana na fedha haramu
i.the
establishment of the Permanent Commission of Inquiry, or Ombudsman, 1966;
ii.the
Foreign Exchange Control Act 1966;
iii.the
Anti-Corruption Act 1971;
iv.the
establishment of an anti-corruption squad in 1975;
v.the
Economic Sabotage Act 1983;
vi.the
Economic and Organised Crime Act 1984;
vii.the
Proceeds of Crime Act 1991;
viii. the
Leadership Code (Declaration of Assets) Act 1995;
ix.the
appointment of the Presidential Commission of Inquiry into Corruption,1996;
x.the BOT
Circular to Banking and Non-banking Financial Institutions, No. 8of 2000, on
Money Laundering.
xi.the
Drugs and Illicit Traffic of Drugs Act 1995;
xii. the
Arms and Ammunition Act 1991;
xiii.the
Mutual Assistance in Criminal Matters Act 1991; and
xiv.the
Tanzania Intelligence and Security Act 1998.
xv.The
anti-money laundering Act, 2007
xvi.the
anti-money laundering (amendment) act, 2012.
No comments:
Post a Comment