Mkurugenzi wa manispaa ya moshi mkoani Kilimanjaro,
Bernadette Kinabo
amewataka madereva wanaoingiza magari yao katika stendi kuu
ya mabasi
moshi kulipa ushuru uliongezeka na kuacha kulumbana kwa kuwa
kiwango
kilichoongezwa hakita badilishwa.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusiana
na
madereva wanaoingiza magari katika stendi na kukataa kulipa
ushuru kwa
madai kuwa ushuru huo umeongezwa bila kushirikisha madereva
hao,
Kinabo amesema kiwango hicho hakitabadilishwa na wanatakiwa
kulipa ili
manispaa iweze kujenga barabara zote kwa kiwango cha lami.
Kinabo amesema madereva hao wanakataa kulipa kutokana na
wakala
aliyepewa tenda ya kukusanya ushuru ndani ya manispaa hiyo
kushindwa
kusimamia zoezi la kupanga magari na kukusanya ushuru huo.
Mkurugenzi huyo amesema zoezi hilo limekwama kutokana na
wakala
aliyepewa tenda hiyo kushindwa kupanga magari na kutoza
ongezeko hilo
na kwamba manispaa inaweka wakala mwingine ambaye ataweza
kusimamia zoezi la kutoza viwango vya ushuru vilivyoongezeka.
Nao baadhi ya madereva hao ambao ni Daniel Kimwaga, Muhamed
bonge
na Mwidoe Rajabu wamesema hawatalipa kiwango hicho na badala
yake
watalipa kiwango cha zamani ambacho walichokubalina na
manispaa hiyo
kutokana na manispaa kutowashirikisha madereva hao kuhusiana
na
mabadiliko ya ushuru huo.
No comments:
Post a Comment