Mwalimu wa shule ya msingi, Daniel Lukindo mwenye umri wa miaka 24,
amekukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela baada ya kupatikana na hatia
ya kumpa mimba mwanafunzi, Halima Rashidi, wa kidato cha nne katika
shule ya sekondari ya Kwaluguru.
Kimaadili, sitetei alichokifanya, ila kisheria ni sawa kwa mtu kwenda
jela kwa kufanya mapenzi na mwanafunzi wa kidato cha nne? Sijui kama
umri umebadilika siku hizi lakini tulipokua kidato cha nne, mimi na
wanafunzi wenzangu wote tulikua na umri kati ya miaka kati ya 16 na 18.
Ingawa tulikua wanafunzi, tayari tulikua watu wazima na tulijua mabaya
na mazuri, na tulijua tunachokifanya. Nilivyodhani mimi, sheria kama
hizi ni za kuwalinda wasichana/wavulana wenye umri mdogo ambao
hawajapevuka kiakili; lakini kwa mtu aliyekua kidato cha nne, akipata
mimba ni uzembe wake maana ana umri wa kutosha kujua anachokifanya. Na
sidhani kama kazi ya sheria ni kulinda uzembe wa watu. Au mnaonaje? Na
kama mwl. Lukindo anakwenda jela kwa miaka mitatu, je huyo msichana naye
ataadhibiwa maana na yeye alishiriki katika tendo hilo na ana umri wa
kutosha kutambua athari za anachokifanya?
Anyway, back to the story, akisoma mashtaka katika shauri hilo,
Mwendesha Mashtaka, Mkaguzi Msaidizi wa Polisi Elibaliki Polanjo,
aliiambia mahakama kuwa kati ya Novemba mwaka jana na Februari mwaka huu
katika Kijiji cha Magamba, mwalimu huyo, wa shule ya msingi ya Magamba
iliyopo Handeni, Tanga, alikuwa akifanya mapenzi na mwanafunzi huyo na
baadaye, kumpa ujauzito.
Katika kesi hiyo iliyokuwa chini ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama
ya Wilaya ya Handeni, Patrick Maligana, mshtakiwa alikiri kosa lake,
akikubaliana na maelezo yote yaliotolewa na mwendesha mashtaka.
Kufuatia hatua hiyo, Hakimu Maligana, alimtia hatiani na kumhukumu kutumikia adhabu ya kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela.
Akifafanua kuhusu adhabu hiyo, Maligana alisema mshtakiwa alitenda
kosa baya na hasa ikizingatiwa kwamba ni mwalimu anayepaswa kuwa mfano
mzuri katika jamii, kwa kuzuia na kukomesha wimbi la matukio ya
wanafunzi wa kike kupata mimba.
“Sheria inasema mwanaume yeyote atakayempa mimba mwanafunzi atakuwa
ametenda kosa na kama atapatikana na hatia, atastahili kutumikia kifungo
kisichopungua miaka mitatu jela na kisichozidi miaka sita. Kwa
hiyo sheria hiyo inalinda wasichana kutokana na status yao, ya kama ni
wanafunzi au la, na sio kutokana na umri wa kuelewa/kutoelewa athari ya
kinadhofanyika? Ina maana ni sawa kufanya mapenzi na msichana wa miaka
14 asiyekuwa mwanafunzi lakini ni kosa kufanya mapenzi na msichana wa
miaka 18 aliyekua mwanafunzi? Naomba mnielimishe mnaoelewa sheria hii
maana kwangu it doesn’t make sense at all)
Kwa Kosa hili halitakuwa na nafasi ya kulipa faini,” alisema
Maligana. Aliongeza kuwa adhabu hiyo itakuwa fundisho kwa walimu na
wanaume wengine wenye tabia ya kupenda kufanya mapenzi na wanafunzi wa
kike. (Vipi kuhusu mwalimu wa kike akifanya ngono na mwanafunzi wa kiume enh? Sheria hapo inasemaje? Hmm?)
No comments:
Post a Comment