Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, September 15, 2012

MWANDISHI AFUKUZWA UANACHAMA BAADA YA KUWASALITI WENZAKE...!


MUSOMA
CHAMA cha Waandishi wa Habari mkoani Mara MRPC, kimemfukuza uanachama wa chama hicho, mwandishi wa habari wa radio Free Afrika mkoani Mara Bw Maxmilian Ngesi baada ya kukiuka makubalino ya chama hicho yaliyofikiwa juzi ya kutoandika kabisa habari za jeshi la polisi mkoani humo.

Akizungumzia kufukuzwa kwa Mwandishi huyo mwenyekiti wa chama hicho Bw Emmanuel Bwimbo,alisema kuwa Ngesi amekiuka makubaliano ya waandishi wenzake na chama kwa ujumla baada ya kusikika akitangaza habari za jeshi la polisi kwa kumkariri kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara.

“ Sisi kwa kauli moja tumekubaliana kutofanya kazi na Jeshi la Polisi Mkoani Mara baada ya Matukio kadhaa likiwemo ya kuuawa kwa mwandishi wa habari mkoani Iringa na kutunyima kibali cha Maandamano yetu ya Amani kupinga Mauaji hayo” alisema Bw Bwimbo

Bw Bwimbo alisema kuwa kitendo hicho kinaonyesha jinsi gani mwandishi huyo alivyokiuka makubaliano ya pamoja na kuwasaliti wenzake ambao wamekubaliana kwa pamoja kuwa hawataandika habari za jeshi hilo kutokana na kuzuiwa waandishi kutoandamana katika maandamano ambayo yaliitishwa nchini kote kulaani kitendo cha mauaji ya mwandishi wa kituo cha chanel Ten mkoani Iringa Daud Mwangosi.

Alisema Ngesi kama mwanachama alitakiwa kutii maamuzi ya chama na tamko la chama chake kwa vile tamko hilo limewataka wananchama wote na siyo kwa mkoa wa Mara tu lakini pia baadhi ya mikoa imetoa matamko na misimamo hiyo lakini cha kushangaza yeye amekaidi na kwenda kinyume.

Aidha Mwenyekiti huyo alisema kamwe chama hicho hakiwezi kuvumilia mwandishi atakaye kiuka agizo hilo na hatua ambayo imechukuliwa kwa Ngesi ni mfano kwa waandishi wengine hadi hapo tamko hilo litakapo tenguliwa.

Jumatatu wiki hii waandishi wa habari walifanya maandamano nchi nzima wakilaani mauaji ya mwandishi mwenzao Daudi Mwangosi ambapo kwa mkoa wa Mara maandamano hayo yaliuzuiwa na polisi hali iliyofanya chama cha waandishi wa habari kukataa kuandika habari za jeshi hilo mkoani Mara.

No comments:

Post a Comment