Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, October 30, 2012

DIWANI AWATAKA WATENDAJI WA SERIKALI ZA MITAA KUJISHUHULISHA...!

 Zainab Maeda, Iringa.

       WATENDAJI wa serikali za mitaa wamewatakiwa kujishughulisha na shughuli mbalimbali za kijamii ili kuleta maendeleo. Sambamba na hayo Diwani wa kata ya Mtwivila aliwataka kutokuwa na kauli za uwongo wakati wakipigiwa simu na viongozi wa juu au wananchi.

       Aliyabainisha hayo, Diwani wa kata ya Mtwivila manispaa ya Iringa,
Vitus Sabas Mushi wakati wa mkutano wake pamoja na watendaji hao kilichofanyika kwenye  ofisi ya mtendaji katika kata hiyo.

         Mushi alisema kata hiyo inamazingira machafu hali ambayo yanaeza
kusababisha mlipuko wa magonjwa, pia kata hiyo inakabiliwa na uhaba wa maji .

       Alifafanua kuwa wanampango wa kuboresha ofisi ya kata hiyo pamoja na
barabara zilizopo kwa kuweka matuta madogo na makubwa ili kuzuia ajali ambazo zinasababishwa na mwendo kasi wa magari.

      Wakati akihojiwa na chanzo chetu  mtendaji wa kata hiyo Angela Mtimwa
alisema lengo kuu la mkutano huo ni kujadili mambo mbalimbali kama ujenzi wa kituo cha polisi, ukarabati wa ofisi hiyo ya mtendaji ujenzi wa kituo cha afya, mfuko wa elimu pamoja na ukusanyaji wa mapato.

      Aidha alisema changamoto mbalimbali wanazokutana nazo ni wakati wa ukusanyaji wa
mapato wananchi hawapatikani katika maeneo yao hali ambayo inawalazimu kutumia gharama kubwa kwa kuwatafuta wanaohusika na majengo hayo kwa kuwapigia simu.

No comments:

Post a Comment