Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, October 13, 2012

KAMANDA WA POLISI WA MKOA WA MWANZA AUWAWA KWA KUPIGWA RISASI NA MAJAMBAZI...!

Liberatus Barlow wakati wa uhai wake
 
Mkuu  wa  jeshi la  polisi (IGP) Said Mwema amethibitisha  kuuwawa kwa kakamnda  wa  Mwanza Liberatus Barlow .

Amesema  kuwa  kamanda  huyo wa polisi ameuwawa na  watu  wanaosadikika kuwa ni majambazi majira ya saa 7.30  na saa 8 usiku   katika maeneo ya Kitangiri jijini Mwanza.

Mwema amesema  kuwa kamanda  Barlow alikuwa akitokea katika  kikao cha harusi akiwa njiani kumrudisha dadake nyumbani kwake ghafla  alikutwa na tukio  hilo la  kupigwa  risasi.

Hata  hivyo alisema  kuwa  kutokana na tukio  hilo jeshi la  polisi  linataraji kuanza uchunguzi  wake kuanzia leo na timu ya askari  kutoka  makao makuu ya polisi  wataondoka mapema leo kwenda  jijini Mwanza  kuungana na askari wa mkoa  huo kwa ajili ya uchunguzi  zaidi na msako wa majambazi hayo .

Mwema amewataka  wananchi  wa Mwanza  kutoa ushirikiano wao kwa  jeshi la polisi ili kufanikisha  zoezi hilo na  kuwataka kutokuwa na hofu  yoyote kutokana na tukio  hilo.

No comments:

Post a Comment