Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, October 11, 2012

WAFANYA BIASHARA WA SOKO LA MAKETE WAMUOMBA MKURUGENZI WA SOKO WATUMIE USHURU WANAOTOZWA KUJENGEA CHOO...!

Wafanyabiashara katika eneo la sokoni wilayani Makete wamemuagiza Mwenyekiti wa soko hilo Bw. Hosea Mpandila na viongozi wenzake kwenda kumuona mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo na kumwambia kuwa wanaomba awasamehe kulipia ushuru wa biashara zao kwani wanaelekeza fedha zao katika ujenzi wa Choo sokoni hapo

Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika sokoni hapo, wafanya biashara hao wamesema, kutokana na choo wanachokitumia hivi sasa kujaa, wanalazimika kujenga choo kingine mara moja hivyo wanamuomba mkurugenzi awasamehe kulipia ushuru mpaka wamalize kujenga choo hicho

Katika mkutano huo wafanyabiashara hao wameamua kuwa kila mmoja wao alipie mchango wa tsh. 10,000/= kwa ajili ya ujenzi huo mchango unaotakiwa ulipwe mara moja

Mmoja wa wafanyabiashara hao aliyejitambulisha kwa jina la Mia amesema kutokana na ulazima wa kuchangishana fedha kwa ajili ya ujenzi wa choo sokoni hapo, gharama ya shilingi 10,000/- ni kubwa hivyo wanamuomba Mkurugenzi kuwasamehe ushuru wa sh. 1,500/- hadi hapo watakapomaliza ujenzi huo

Suala la kwenda kumuomba mkurugenzi awasamehe kulipia ushuru lililimtia hofu mwenyekiti wa soko Bw. Hosea Mpandila ya kwenda kumuomba mkurugenzi kwa madai kuwa huenda asikubali jambo lililowafanya wafanyabiashara hao kumuagiza kuwa ni lazima aende

“Sisi ndio tumekutuma na lazima ukatekeleze maana wewe unafanya kazi na sisi na tunapokuwa na kero zetu lazima uzifikishe kunakohusika, wewe unachoogopa nini wakati tuliokutuma ni sisi?” alisema Mia

Katika kikao hicho wamechaguliwa wajumbe wanne kushiriki kwenye kamati mbili ambazo ni kamati ya fedha na ya ujenzi ambapo zote zina wajumbe wanne na zimeagizwa kuanza kazi mara moja

Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na mgogoro wa ujenzi wa vyoo ingawa choo cha soko hilo kilikuwa kimejaa muda mrefu, na ujenzi wa vyoo hivyo huenda ukawa mkombozi wa tatizo hilo

No comments:

Post a Comment