Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Tuesday, November 6, 2012

CCM: Makovu ya kura za maoni yametugharimu..!

Makovu ya kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) yamezidi kukitesa chama hicho baada ya tathmini kuonyesha kuwa makundi yaliyotokana na uchaguzi huo ndiyo yaliyosababisha kushindwa udiwani kwenye kata saba.
Katika uchaguzi uliofanyika katika kata 29, CCM kilishinda kata 22 na kupoteza kata saba ambazo zilikwenda kwa vyama vya Chadema, TLP na CUF.
Akizungumza katika mkutano wa kuwashukuru wananchi kwa kumchagua diwani wa CCM katika Kata ya Msalato, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake wa CCM (UWT), Amina Makilagi, alisema hayo yalibainika katika kikao cha tathmini kilichofanywa na Sektarieti ya Halmashauri Kuu mjini hapa juzi.
Makilagi ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalum, alisema walibaini utaratibu wa kura za maoni ambao unataka mshindi kuwa na zaidi ya nusu ya kura zote za wapiga kura ulisababisha makundi.
“Siyo kwanza tulishindwa katika kata hizo kwa sababu CCM haipendwi, bali tumebaini kuwa utaratibu ule wa kumpata mshindi kwa zaidi ya nusu ya kura zote zinazopigwa unafaa kutumika katika chaguzi za ndani ya chama,” alisema.
Alisema katika baadhi ya kata hizo baada ya uchaguzi kurudiwa kwa mara ya pili, alipatikana mshindi mwingine na hivyo kusababisha makundi.
“Haya makundi yalisema bora tukose wote ndio maana tukashindwa siyo kwamba wananchi walikuwa wakivitaka vyama hivyo,” alisema.
Matokeo ya uchaguzi huo wa Oktoba 27, mwaka huu Chadema kilishinda katika kata tano na kukifanya kuongeza madiwani watatu. TLP na CUF kila kimoja kilipata kata moja.
CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment