Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, January 31, 2013

BREAKING NEWS: TAARIFA KUHUSU JAHAZI LILILOZAMA NUNGWI LEO JANUARY 31 2013 LIKIWA NA WATU 32...!

Hili ndio Jahazi liitwalo Sunrise lililozama kwenye eneo la Nungwi.

TAARIFA zilizoteka vyombo vya habari kwa sasa ni kuhusu kuzama kwa Jahazi liitwalo Sunrise likitokea Tanga kulekea visiwani Zanzibar likiwa na abiria 32 ambapo limezama kwenye lile eneo la Nungwi ambalo ni hatari siku zote.


Namkariri Kamanda wa Polisi Zanzibar akisema “tayari tumeshapokea watu 21 waliookolewa wakiwa wazima na hakuna maiti iliyopatikana mpaka sasa hivi, waliokuwemo kwenye chombo ni watu 32 hivyo watu bado watu 11 hawajulikani walipo”

Endelea kuisikiliza Clouds Fm pamoja na kupita hapa millardayo.com kwa taarifa zaidi zitakazotufikia wakati wowote

No comments:

Post a Comment