Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, January 31, 2013

HIVI NDIVYO VIWANGO VYA PUNGUZO LA KUPIGA SIMU KWA MITANDAO YA TZ, MARCH 2013, JAN 2014, 2015 NA 2016

 

 

Mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA imeyataka makampuni ya simu za mkononi Tanzania kuhakikisha yanaanza rasmi mpango wa punguzo la bei ya kupiga simu katika mitandao mingine kutoka bei inayotumika sasa hivi ya shilingi 113 kwa dakika mpaka shilingi 34 na senti 92 ikiwa ni bei mpya inayotakiwa kuanza kutumika kuanzia siku ya kwanza ya mwezi March 2013.

 

Mkurugenzi Mtendaji wa TCRA Profesa John Nkoma amesema uamuzi wa kufanya hivyo ni kutokana na kupanda kwa gharama za maisha ambapo makampuni hayo yanatakiwa kuanza utekelezaji wa agizo hilo na hatua za kisheria zitachukuliwa kwa kampuni yeyote ambayo itafanya kinyume na hayo maagizo.

Namkariri akisema “bei itaendelea kushuka kadri miaka inavyokwenda, tarehe 1 january 2014 bei itatakiwa kuwa sh 32 na senti 40, tarehe 1 january 2015 sh 30 na senti 58, tarehe 1 january 2016 itatakiwa kuwa sh 28 na senti 57, hizi bei ni za juu kabisa na Kampuni za simu ni ruksa kwao kuzungumza na wakatumia bei ya chini kabisa”

No comments:

Post a Comment