Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Sunday, May 5, 2013

BREAKING NEWZZ: KANISA KATOLIKI LALIPULIWA NA BOMU JIJINI ARUSHA LEO ASUBUI...!

Taarifa  zilizotufikia  hivi  punde  ni  kwamba  bomu  limelipuka  katika  kanisa  katoliki, parokia  mpya  ya Olasiti iliyokuwa  inazinduliwa  leo  jijini  arusha. Bomu  limelipuka  wakati  waumini  wa  kanisa  la katoliki wakijiandaa  na  misa  ya  uzinduzi  wa  parokia  hiyo. 
 
Ambapo mpaka  sasa  haijajulikana  idadi  kamili  ya  watu  waliojeruhiwa  ama  kupoteza  maisha  lakini taarifa  za  awali  zinasema  kuwa  baadhi  ya  majeruhi  wamekimbizwa  hospitali.

Chanzo  cha  mlipuko  huo  inasemekana   kuwa  kuna  gari  ndogo   ilifika  kanisani  hapo  na  kusimama.
Baadae  alishuka  mtu  aliyekuwa  amevalia  vazi  mithili  ya  kanzu  na  kurusha  kitu  kuelekea  kanisani  ambacho  ndicho  kilichosababisha  mlipuko  huo.
Mgeni rasmi   katika  uzinduzi   huo  alikuwa  ni   balozi wa Vatican nchini Tanzania. Ambapo yupo baada  ya kunusurika  katika  mlipuko huo wa bomu.
 
Timu nzima ya mtandao huu wa www.kingjofa.blogspot.com unawapa pole sana wamini wote wa kanisa la katolini na pia watu wote walioguswa na kitondo hicho cha kinyama.

 Hizi ni taarifa za awali tu lakini kwa taarifa zaidi kuhusiana na mlipuko huo endelea kutembelea mtandao huu wa www.kingjofa.blogspot.com

No comments:

Post a Comment