Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, May 4, 2013

DJ VIRUS: NI DJ MWENYE UMRI MDOGO ILA MWENYE UWEZO MKUBWA SANA KIUTENDAJI...!

    

Mohamed Waziri maarufu kama DJ Virus.

   Leo nipo na Mohamed Waziri maarufu kama DJ Virus ni  maarufu sana ukanda wa kaskazini mwa Tanzania hususani katika mkoa Kilimanjaro kiukweli ni DJ mwenye umri mdogo lakini ana uwezo mkubwa sana katika kufanya kazi ya u’DJ kazi ambayo inahitaji umakini wa hali ya juu. DJ Virus alianza kufanya kazi ya u’DJ kwenye club ndogo ndogo za mjini Moshi miaka ya 2007 wakati akiwa shule ya secondary na hakupenda kuishia hapo maana alikua na imani kubwa sana na kazi hii ambayo aliiipenda na pia aliahidi kuitendea haki kazi hii ya u’DJ kwa kuwa aliamini ni kazi ambayo inaweza kumletea mafanikio makubwa katika maisha yake.
 
DJ Virus kwa sasa ni DJ katika radio inayofaamika kama Kibo Fm iliyopo wilaya ya Hai - mjini Moshi pia anafanya kwenye baadhi ya Club na kwenye matamasha mbalimbali amekua akifanya kazi hiyo na anasema kwa mtu yeyote akimuhitaji kwa ajili ya kufanya show sehemu yoyote yeye yupo tayari kikubwa ni kuwasiliana na uongozi wa Kibo Fm na kuweka utaratibu mzuri ambao hautaweza kuadhiri ratiba zake wala ratiba za ofisini (Kibo Fm). Baada ya kunielezea hayoyote sikupenda kuishia hapo bali nilitamani pia kufahamu mambo mengi hususani yanayogusa tasnia ya burudani na wadau wa burudani pia.

Nilimuuliza ni nyimbo za aina gani ambazo ukizipiga unahisi kama watu wengi sana wanazipenda na kuzifurahia? “actually dj kama dj anatakiwa apige nyimbo zote kwani watu wanaosikiliza ngoma ni wengi sana kila mtu anatamani kusikia ladha yake ila kiukweli ki bongo bongo watu wanapenda sana bongo flavour” Alijibu DJ Virus

Kwa hapa mkoa wa Kilimanjaro unahisi kama producers, wasanii na watangazaji au maDJs mnaushirikiano mzuri kwenye kufanikisha harakati za muziki? “Hapa mkoani banaaa kiukweli ma dj ma presenter na ma producer hawana ushirikiano kila mtu anataka kuwa zaidi ya mwenzake hatuwezi kufika kwa staili hii alafu ma dj wengi wana copy na ku paste hakuna tofauti ya ladha” Alijibu DJ Virus

Wewe kama DJ unadhani kati ya producer na msanii ni yupi anailikupewa lawama endapo nyimbo itakua mbaya? “inategemea coz producer ndo anamsikia msanii kwa mara ya kwanza hivyo yeye ndo anajuwa kuwa msanii yupo vizuri au bado kama bado anapaswa kumrudisha nyumbani akafanye mazoezi tena ya sauti au vitu vingine lakini sasa ivi ma producer nao wapo after money wao hawaangalii tena hivyo vitu bali wao sasaivi wannaangalia mkwanja tu so nyimbo ikiwa mbaya wa kwanza kulaumiwa ni producer” Alijibu DJ Virus

Wewe kama DJ ni juhudi gani binafsi ambazo unazifanya kufanikisha mziki hususani kwa mziki unaofanywa na wasanii wanaotokea mkoa wa Kilimanjaro? “mimi kama mimi nawapa airtime ya kutosha ngoma wanazonipa nazitendea haki sana kiukweli na kuna baadhi ya matamasha makubwa yanatokea pia nawapaga nafasi ya upaform jukwaani ili wazidi kujulikana na pia wanapewa kipato kidogo kama kupewa big up kwa alichokifanya jukwaani” Alijibu DJ Virus

Kuna lawama kwamba nyie ma DJ wa radio za hapa mkoani Kilimanjaro huwa hamzipi airtime ya kutosha ngoma za wasanii wa nyumbani (Kilimanjaro) mpaka wasanii wawape hela? “Hahahaaaaaa amna bana ila kiukweli mi sijawahi kupokea hela ya msanii ila wapo baadhi ya wasanii pia walishawahi kuniambia kuwa walishawahi kwenda katika moja ya radio hapa moshi naihifadhi kwa jina jamaaa walitakiwa watoe elfu 20 ili ngoma yao ichezwe radioni na pia wakitaka kufanya interview watoe hela kidogo pia” Alijibu DJ Virus

Huyo alikye hitaji hela anaitwa nani na anafanya kwenye radio gain? Maana ni vyema watu wakamfahamu hususanni wasanii wa mkoa wa Kilimanjaro ili wakiwa na ngoma mpya watafute na 20,000 ili ngoma yao isikike radioni? “hapana nimesema hivyo ili kuondoa misunderstanding” Alijibu DJ Virus

Huoni kwa kuto kumtaja utakua unakumbatia maovu ambayo mwisho wa siku yatazidi kuudididmiza mziki wa vijana wa mkoa wa Kilimanjaro? “Kwa kweli siwezi kumtaja ila wakisikia au wakuisoma habari hii wale wasanii na yule DJ atawza kujirekebisha tabia yake” Alijibu DJ Virus

Nasikia pia nyie ma DJ huwa mkipewa CD na wasanii wadogo mnatabia ya kuwaambia kuwa “MBONA CD IPO EMPTY?” Na msanii anapojaribu kukuelewesha kuwa CD sio Empty huwa mnazidi kusisitiza kuwa CD ni Empty kumbe maana ya CD EMPTY ni kwamba CD HAINA HELA ili ngoma yako ikapate airtime.

Nashukuru sana kwa time yako ila wafikishie salamu ma DJ wote wenye tabia za kudai hela ili wazipe airtime ngoma za wasanii wachanga siao fresh bana, maana wanawakatisha tama na mwisho wa siku pia ma DJ nao wanaharibu vipindi vyao kwa kuacha kucheza ngoma nzuri za wasanii wachanga na kung’ang’ania kucheza ngoma mbaya kwa kuwa zimelipiwa hela..

 Bovya kwenye mshale hapo chini usikiliza Mixing iliyofanywa na DJ Virus

No comments:

Post a Comment