Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, May 27, 2013

WARSHA YA UTENGENEZAJI FILAMU- MAOMBI YAFUNGULIWA...,



 Zikiwa zimesalia Takribani siku 34  ili kuweza kufikia katika Tamasha la kumi na sita la nchi za majahazi lijulikanalo kama Zanzibar International Film Festival (ZIFF) kwa mwaka wa 2013 ambapo linategemewa kuanza mnamo Tarehe 29 ya mwezi wa sita mpaka Tarehe Saba ya Mwezi wa saba mwaka wa 2013.
 Katika kuhakikisha ZIFF inanufaisha watengenezaji wa Film wa nchi za Afrika Mashariki na Kati.
ZIFF sasa inapokea maombi kutoka kwa watengenezaji filamu Afrika Mashariki wanaotaka kushiriki katika warsha ya utengenezaji filamu wakati wa ZIFF mwaka huu..
Wanafunzi 5 (mmoja toka kila nchi ya Afrika Mashariki) watalipiwa safari, malazi na chakula ili kushiriki kwenye warsha hiyo. Wanafunzi 5 wengine watajilipia wenyewe.
Mfumo wa warsha utakuwa ni kufuatilia kikundi cha watengeneza filamu walio tayari mafundi watakaokuwa wanatengeneza filamu fupi wakati wa ZIFF. Utengenezaji huu unaitwa Guerilla Filmmaking (yaani filamu chapchap) na katika siku 6 filamu itapigwa, itahaririwa na kuonyeshwa ZIFF siku ya mwisho.
Wanaotaka kushiriki kwenye warsha watume maombi yao hivi:
CV fupi.
Maelezo kwa nini wachaguliwe (maneno 1000)
Maombi yatumwe kwa: workshop@ziff.or.tz
Warsha imedhaminiwa na Goethe Institute na GIZ (Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa la Ujerumani) na Jumuia ya Africa Mashariki (EAC)
Maelezo pia yako www.ziff.or.tz 

No comments:

Post a Comment