Rachel Haule ‘Recho’.
MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Rachel Haule ‘Recho’ alijikuta
akichezea kibao cha ukweli na kusababisha aangue kilio wakati alipokuwa
akirekodi sinema. Akizungumza na Stori 3, sosi aliyeshuhudia tukio hilo lililotokea
maeneo ya Mwenge, jijini Dar alisema msanii huyo alikuwa katika kurekodi
moja ya vipande vya sinema yake mpya lakini kutokana na matakwa ya
filamu hiyo kuonesha hisia za kulia, ilibidi Baba Haji amshushie kofi
fastafasta.“Siku hiyo sikuwa kwenye ‘mudi’ sababu kuna mambo yalinichanganya, nilishindwa kuvuta hisia za kulia ndipo niliposhtukia kofi la Baba Haji na machozi yalinitoka yenyewe, hii kazi yetu hii we acha tu,” alisema Recho.
No comments:
Post a Comment