Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Thursday, July 25, 2013

Shilole matatani kwa kupotea na simu alizopewa amletee diamond platnumz toka Afrika Kusini.

Shilole matatani kwa kupotea na simu alizopewa amletee diamond platnumz toka Afrika Kusini.
STAA wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Zuwena Mohammed ‘Shilole’ ameingia matatani akidaiwa kuingia mitini na simu tatu za mkononi alizopewa nchini afrika nchini Afrika ya Kusini alikokwenda kufanya shoo global publisher wameripoti.
Habari hiyo inasema kuwa msanii huyo alikumbwa na kasheshe hilo Julai 19, 2013 nyumbani kwa mwanamuziki wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’, Sinza Mori, Dar.
Siku hiyo amabayo Diamond alikuwa akifuturisha na aliwaalika watu mbalimbali wakiwemo mastaa

Habari hiyo inasema kuwa simu hizo alipewa shilole ili amletee diamond tokea afrika ya kusini alipoenda kufanya shoo lakini alipofika hakufanya hivyo.
Katikati ya mzozo huo, Shilole alijitetea kwa kusema: Mi namdai rafiki yake fedha yangu ya shoo iliyobaki, kama shilingi laki nane hivi ndiyo maana nikaamua kuzizuia simu za huyu (Q Boy aliyempa simu hizo) hadi nimaliziwe pesa yangu.
Hata hivyo, katika sakata hilo ilielezwa kuwa Shilole na Q Boy hawakuwa na makubaliano yoyote kuhusu shoo hiyo na simu hizo hivyo madai ya mwigizaji huyo ni ‘usanii’ tu.

Bado tunamtafuta shilole na Diamond kupata ukweli halisi wa tukio hilo.

No comments:

Post a Comment