Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, July 13, 2013

MFAHAMU WISEMAN KIJANA MZALENDO WA KITANZANIA ALIYETEMBEA KWA MIGUU KUTOKA MBEYA MPAKA DAR...!

Jennifer Livigha (Team Leader wa ChingaOne blog - kulia ) akiwa pamoja na mtembeaji maeneo ya Sam Nujoma Road  mara baada ya kuwasili  jijini Dar es salaam akiwa njiani kuelekea Mikocheni kwenye studio za Clouds FM.

Tanzania ni nchi yangu,Taifa Star ni timu yangu, Amka.......Saa ya Uzalendo imefika..... maneno haya yametumika kama kauli mbiu ya Mtembeaji ........ ni maneno yenye  kuleta hamasa kubwa kwenye masikio ya kila mzalendo, ni maneno yenye kuonyesha ari, nguvu na kutia moyo kwa yoyote ambaye ni mzalendo. Ni kijana mwenye nguvu na shughuli zake zinazoweza kumuingizia kipato na kuweza kuishi....... lakini kutokana na uzalendo alionao kwa nchi yake na  mapenzi makubwa aliyonayo kwa timu yake ya Taifa aliamua kufanya safari ndefu ya miguu kutoka Mbeya hadi jijini Dar es salaam akiwa na nia ya kuja kuipa nguvu timu yake ya Taifa star. Watu wengi tunaamini  uzalendo huonekana pale mtu anapojiingiza kwenye siasa, ila hili litabadili fikra za watu na kujua kuwa  uzalendo upo sehemu nyingi ikiwemo hii.....
 Binafsi anasema safari yake  anaiita Uzalendo Tour na nia kubwa  ni kuiunga mkono  timu ya Taifa Stars, anashukuru sana  kwa nguvu aliyoipata toka alipoanza safari yake , watu wengi wamejitokeza sehemu mbalimbali toka Mbeya hadi Dar es salaam na kuweza kumpigia simu, kumpa vitu mbalimbali vilivyoweza kufanya safari yake kuwa rahisi. Wazo lake lilikuwa la muda mrefu sana lakini kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wake alishindwa kulitekeleza kwa wakati huo. Safari ya miguu kwa kilometa nyingi kama hizo sio rahisi kwa yoyote  ila kutokana na Uzalendo wake  ameweza kutimiza ndoto yake, Safari yake amekuwa akiifanya muda wa mchana na giza linapoingia alilazimika kupanda gari..... anamshukuru sana  Gerald Hando wa PowerBreakfast wa Clouds fm kwa moyo na nguvu kubwa aliyoitumia katika kufanikisha safari hii. 
...UZALENDO KWANZA..
 Chanzo: Chingaone.com

No comments:

Post a Comment