Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, August 5, 2013

HUDUMA YA UTOAJI WA TAARIFA ZA WAHAMIAJI HARAMU YAZINDULIWA JIJINI DAR ES SALAAM

clip_image001
Watanzania wametakiwa kuitumia vema huduma mpya ya utoaji taarifa za wahamiaji haramu pamoja na taarifa za waathirika wa biashara hiyo, ili kupata msaada na kupunguza kasi ya biashara hiyo nchini.
Huduma hiyo imezinduliwa leo jijini Dar es Salaam na shirika la kimatiafa la Wahamiaji (IOM) kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Ndani, ambapo Mkurugenzi wa Sera na Mipango wa Wizara hiyo, Haji Janabi ametoa wito wa matumizi sahihi ya huduma hiyo katika kutoa taarifa za wahamiaji haramu pamoja na vitendo vya biashara haramu ya binadamu.
Huduma hiyo ambayo ni kitabu chenye namba za simu za vyombo mbalimbali, vikiwemo vyombo vya dola vinavyotoa msaada wa haraka, imekuja wakati ambapo Tanzania imekuwa ikishuhudia ongezeko la matukio ya wahamiaji pamoja na biashara haramu ya binadamu.

No comments:

Post a Comment