Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, September 28, 2013

MUENDESHA BODABODA AGONGWA NA GARI NA KUFARIKI DUNIA PAPO HAPO..

Marehemu Said maarufu kama "Mwauwezo" akiwa amefunikwa na kanga na wasamaria wema muda mfupi baada ya ajali.
MOSHI Ajali Mbaya iliyosababishwa na Gari aina ya Land cruiser ambayo Dereva wake alikimbia Baada ya Kumgonga muendesha pikipiki (Bodaboda) Katika eneo la Majengo Fire mjini Moshi Mkoani Kilimanajaro Usiku wa jana. Chanzo cha ajali hiyo hakikuweza kufahamika kwa haraka.

Ajali hiyo imepelekea kifo cha Dereva huyo wa pikipiki Aliyetambulika kwa Jina Moja la Said maarufu kama "Mauwezo" mkazi wa njoro mjini Moshi mkoani Kilimanjaro,
analiyesifika kwa Kuendesha Baiskeli kwa umahiri.

Baada ya Ajali hiyo polisi wa usalama barabarani walifika na kuchukua vipimo ndipo kundi kubwa la waendesha bodaboda likajikusanya na kuanza kuharibu gari  lililosababisha ajali na mwishowe wakalichoma Moto huku wakilia kwa sauti kubwa kitendo kolichopelekea Polisi wa Usalama Barabarani kuondoka kwa kuhofu kujeruhiwa na vijana hao waliokua na jazba.
 #teamKINGJOFA

No comments:

Post a Comment