Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, September 28, 2013

Tamasha la Sanaa la Jambo Festival kukutanisha washiriki zaidi ya 100 ndani na nje ya nchi

20130921_141649
 Mwenyekiti wa tamasha la Jambo Festival 2013, 
Bw. Augustine Namfua.
Na.Mwandishi wetu.

ZAIDI ya  washiriki 100 kutoka ndani na nje ya nchi wanatarajiwa kushiriki kwenye tamasha la Sanaa na utamaduni la Jambo Festival litakalofanyika oktoba 23 hadi 27 mwaka huu katika viwanja vya Suye vilivyopo mjini Arusha.

 Mwenyekiti wa tamasha hilo la Jambo Festival 2013 Bw. Augustine Namfua alisema kuwa tamasha hilo ni la pili kufanyika mkoani Arusha ambapo wamekuwa wakifanya kila mwaka lengo likiwa ni kuwawezesha  washiriki mbalimbali kuweza kuonyesha bidhaa zao za kitamaduni kutoka ndani na nje ya nchi.

Alisema kuwa tamasha hilo ambalo ni la kimataifa pia litawashirikisha washiriki kutoka nchi za Ufaransa na Angentina ambao wataweza kuonyesha matamasha mbalimbali ya kitamaduni sambamba na kuonyesha bidhaa zao za kitamaduni.

Alisema kuwa, tamasha hilo litaenda sambamba na matukio mbalimbali ya kiasili ikiwemo maonyesho  ya mavazi ya kiasili,pamoja na tamasha la kiasili kutoka vikundi jijini Tanga, Arusha,  na Dar es Saalamu.

 Namfua aliongeza kuwa, pia kutakuwepo na tamasha la muziki wa kisasa    pamoja na onyesho la  mavazi , na ubunifu wa mavazi ambapo  katika tamasha hilo kwa siku hizo kila siku kutakuwa na matamasha mbalimbali ambayo yatakuwa yakionyeshwa.

 Aliongeza kuwa, tamasha hilo limekamilika kwa asilimia 50 huku watu mbalimbali wakiwemo binafsi, mashirika na taasisi mbalimbali zinazohusika na maswala ya sanaa na tamaduni wanaendelea kujitokeza kwa wingi kwa ajili ya kushiriki katika tamasha hilo.

"Tamasha la mwaka jana lilifana sana kwani tuliweza kupata washiriki wengi sana kutoka ndani na nje ya nchi na lilikuwa na mwitiko mkubwa sana , huku watu mbalimbali wakipata fursa ya kuonyesha sanaa zao na tamaduni mbalimbali na kuweza kujifunza kutoka kwa wenzetu wan je ya nchi ndio maana tumeamua kufanya tena mwaka huu mwezi wa kumi hivyo tunatarajia  watu mbalimbali kushiriki kikamilifu katika tamasha hilo" alisema Namfua.

 Aidha aliwataka watu mbalimbali kufika katika tamasha hilo na kuonyesha  bidhaa zao za kitamaduni zinazotengenezwa kwa mikono pamoja na kutangaza tamaduni zao za kiafrika , huku akiwataka wadau mbalimbali kuonyesha  moyo katika kusaidia matamasha hayo  ili yaendelee kufanyika mara kwa mara.

Credit: Mo Blog

No comments:

Post a Comment