Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Saturday, October 19, 2013

SERIKALI YATAKIWA KUTOA MAELEZO YA UBOVU WA JENGO LA OFISI YA MKUU WA WILAYA YA SIHA.

MOSHI serikali wilayani Siha mkoani Kilimanjaro imetakiwa kutoa maelezo yenye vielelezo vya kutosha kwa maandishi kuhusu ubovu wa jengo la ofisi ya mkuu wa wilaya hiyo ambalo limemlazimu mkuu huyo kuhamia jengo jinguine  la idara ya maji ilikupisha ukarabati.

Agizo hilo limetolewa na kamati ya kudumu ya bunge ya tawala za mikoa na serikali za mitaa wakati wa majumuisho ya ukaguzi wa miradi ya maemdeleo wilayani hapo.

Mwenyekiti wa kamati hiyo Mh. Jonh Iwanji amesema kamati hiyo imetoa siku saba kwa serikali wilayani hapo kuwasilisha taarifa mbele ya kamati hiyo kwaajili ya kuchukuliwa hatua stahiki zaidi.

Naye mkuu wa wilaya ya hiyo Dr. Charles Mlingwa amekiri kuhama katika jengo hilo baada ya wataalamu kutoka chuo kikuu kupitia wakala wa ujenzi wa majengo  ya serikali  nchini kumwagiza aondoke ili kupisha ukarabati wa jengo hilo lililokuwa likihatarisha usalama wake.

Kwa upande wake kaimu meneja wa wakala wa ujenzi wa majengo ya serikali mkoani Kilimanjaro Bw. Audax Ngimbwi amesema mkandarasi wa jengo hilo ni JKT  Suma  na tayari hatua za awali zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kuagizwa kulikarabati  jengo hilo.

No comments:

Post a Comment