Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, October 9, 2013

UUNDWAJI WA BODI ZA MISHAHARA KISEKTA ITAONGEZA TIJA SEKTA BINAFSI.

IMG_6502
Msemaji toka Wizara ya Kazi na Ajira Bw.Ridhiwan Wema(Kulia) akieleza kwa waandishi wa habari kuhusu majukumu ya Bodi  za Mishahara Kisekta kwa mujibu wa sheria Na. 7 ya Mwaka 2004 ya Taasisi za Kazi katika Sekta Binafsi, wakati wa Mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari(MAELEZO) Leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mchumi Mwandamizi wa Wizara hiyo Bw. Jofrey Mashafi.

IMG_6503
Afisa Kazi Mwandamizi toka Wizara ya Kazi na Ajira(kulia) akieleza kwa waandishi wa habari(Hawapo pichani) jinsi ukuaji wa sekta unavyochangia kuanzishwa kwa bodi ya Mshahara kwa Sekta husika wakati wa Mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Leo jijini Dar es Salaam. Msemaji Wizara hiyo  Bw.Ridhiwan Wema.

IMG_6521
Mchumi Mwandamizi toka Wizara ya Kazi na Ajira Bw. Jofrey Mashafi (kulia) akieleza mipango ya serikali ya kukabiliana na tatizo la upungufu wa Ajira Nchini ikiwa ni pamoja kuanzisha programu ya miaka 3 inayoratibiwa na Wizara ya Kazi na Ajira kwa kushirikiana Chuo cha Sokoine na  Bank ya CRDB ya kuwajengea uwezo wahitimu wa vyuo vikuu, inayotarajiwa kuzalisha ajira 30,000, wakati wa Mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Leo jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Afisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bi. Georgina Misama. (Picha na Frank Mvungi-MAELEZO).

Credit: MoBlog 

No comments:

Post a Comment