Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Monday, March 3, 2014

TANESCO HATARINI KUFILISIWA..,






Dar es Salaam. Wakati Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) likipandisha bei ya umeme kwa zaidi ya asilimia 40, limetakiwa kulipa zaidi ya Sh844.8 bilioni, kwa kampuni zilizoifungulia kesi mbili tofauti kwa kukiuka mkataba wa kukodisha mitambo ya kuzalisha umeme ya Kampuni ya IPTL.
Baada ya shirika hilo kushindwa kesi hiyo, sasa limepoteza pia haki ya kumiliki mitambo ya IPTL ikiwa ni mwaka mmoja tu kabla ya muda wa kuikodisha ufikie kikomo na mitambo hiyo iwe mali ya Tanesco kwa asilimia 100.
Mkataba huo wa kukodisha mitambo hiyo wa miaka 20 ulioingiwa mwaka 1995, ulikuwa ufikie kikomo mwaka 2015.
Kiasi hicho cha fedha ni sawa na kiasi cha fedha ambazo kinapangwa kwa ajili ya bajeti za wizara nyeti nchini.
Wakati Tanesco ikitakiwa kulipa deni hilo la Sh884.5 bilioni, mapato yake kwa mujibu wa bajeti ya 2012/2013, ni kati ya Sh60 bilioni na Sh70 bilioni kwa mwezi, huku matumizi yake yakiwa Sh11 bilioni.
Taarifa ambazo gazeti hili limezipata, zinaeleza kuwa Tanesco ilikuwa na kesi mbili, moja iliyofunguliwa jijini Dar es Salaam na nyingine Washington DC nchini Marekani.
Kwa upande wa kesi ya jijini Dar es Salaam, hukumu yake ilitolewa na Jaji John Utamwa wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Januari 17 mwaka 2014 saa 8:30 usiku.
Hukumu hiyo imeanza kuzua maswali mengi kiwa baadhi ya watu wakihoji kwa nini itolewe usiku na siyo mchana.
Hukumu nyingine ni ile iliyotolewa Februari 12 mwaka 2014 na Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji cha Washington DC nchini Marekani.
Katika kesi ya jijini Dar es Salaam, mdai alikuwa ni VIP Engineering and Marketing LMT pamoja na Independent Power Tanzania (IPT).
Wajibu madai katika kesi hiyo walikuwa ni Pan Africa Power Solutions T (LTD), Benki Kuu ya Tanzania ambako Tanesco walikuwa wamefungua akaunti maalumu (ESCROW Account), Stanbic Tanzania Ltd pamoja na UBL Bank Tanzania LTD.
Kwenye kesi ya Washington, Standard Charted Bank (Hong Kong) Limited, iliishtaki Tanesco kwa kukiuka mkataba wa kushindwa kuwalipa ushuru wa Dola za Marekani 2.5 milioni kila mwezi.

No comments:

Post a Comment