Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Friday, May 23, 2014

Kanisa La KKKT Likishirikiana na NCA Wamefanikiwa Kuwezesha Vikundi Zaidi Ya 120 Mkoani Kilimanjaro

Kanisa la KKKT dayosisi ya kaskazini kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la misaada kwa nchi za Afrika, NCA lenye makao yake makuu  nchini  Norway ,wameanzisha jumla ya vikundi vya wajasiriamali 120 mkoani  Kilimanjaro kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kiuchumi ili waondokane na umaskini .

Akiongea wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa viongozi wa vikundi hivyo, yaliyofanyika wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, katibu mkuu wa dayosisi hiyo Bw. Julius Mosi amesema >> "vikundi hivyo vilianza kuandikishwa  mwaka 2008 ,hadi sasa  vina mtaji wa zaidi ya pesa za kitanzania  milioni 250 zikiwa ni fedha ambazo wanachama wamechangishana wao wenyewe."

Bw. Mosi amesema, >> "vikundi hivyo vimeanzishwa bila kuwa na itikadi za kidini wala za kisiasa na kwamba tangu kuanzishwa kwa mpango huo jamii imenufaika katika maswala mbalimbali ya kiuchumi hali ambayo imewawezesha kuondokana na umaskini na kuishi  maisha yaliyo bora ukilinganisha na maisha yao ya awali".

 Mchungaji Andrew Munisi ni mratibu wa vikundi hivyo ambapo amesema kupitia mpango huo vikundi hivyo vinapatiwa semina mbalimbali zikiwamo za kuhusu utawala bora na utunzaji wa mazingira ambapo wanapokutana kila wiki wanapanda  miti  katika maeneo maalumu.

Akifunga mafunzo hayo kaimu mkurugenzi wa wilaya ya Hai Bw. Edward Ntakiliho, amewataka wanasemina hao kuwa mabalozi wazuri, katika kuieneza elimu waliyoipata kwa wenzao pia kuwa makini kwa kutoa taarifa kunako husika pindi wanapobaini hujuma, ama kasoro katika vikundi vyao.

No comments:

Post a Comment