King Jofa
Babi D'e Conscious
Mark Denning
Kutoka kushoto ni Chriss luu, Jasson Nelly, Emmanuel deusdedit na Frank sailo.
Kutoka kushoto ni Frank Ben CEO wa Reflections Media akiwa na Chriss luu pamoja na Jasson Nelly
Ni habari ambayo imechukua nafasi kubwa sana katika vyombo mbalimbali vya habari duniani baada ya tukio la Dani Alves kurushiwa ndizi na shabiki wa Villareal wakati wa mechi na Barcelona. Kitendo ambacho kinatafsiriwa kuwa mtu kurushiwa ndizi ni ubaguzi wa rangi na kwamba nyani ndio wanakula ndizi.
Jambo lililowashangaza wengi ni kwamba baada ya Dani kurushiwa ndizi akiwa uwanjani aliichukua ndizi ile na kuila na
kuendelea na mechi bila hata kujali kelele za mashabiki.
Kutokana na kitendo kile tumeona wanamichezo, wanasiasa, wasanii, na watu wengine wengi wakila ndizi ikiwa ni ishara ya kupinga ubaguzi wa rangi.
Je wewe unapinga ubaguzi wa rangi? Kama ndio ni wakati wako wa kupiga picha ukiwa unakula ndizi na kuituma kwenye email ya kingjofa@gmail.com na picha kumi za kwanza zitawekwa kwenye blog hii ya www.kingjofa.blogspot.com
Tuungane Pamoja Kupinga Ubaguzi wa Rangi Dunia Nzima
No comments:
Post a Comment