Banner

Banner

FOLLOW US FACEBOOK

propertyfinder.co.tz

Wednesday, May 28, 2014

MFANYA BIASHARA AJIUWA KWA KUJIPIGA RISASI.

MOSHI mfanyabiashara mmoja ambae ni mkazi wa kijiji cha Kindi  Msasani wilayani Moshi mkoani Kilimanjaro amejiua kwa kujipiga risasi shingoni mara badaa ya kuugua kwa muda mrefu.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kaimu kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Koka Moita alisema tukio hilo lilitokea tareh 27 Mei 2014 majira ya saa 1:15 asubuhi katika kijiji cha Kindi  Msasani.

Koka Moita alisema kuwa mfanyabiashara huyo aliyefahamika  kwa jina la Wararimbo  Lema mwenye umri wa miaka 74 alichukua uamuzi huo wa kujipiga risasi akiwa nyumbani kwake mara  baada ya kuugua kwa muda mrefu. .

Moita alisema kuwa >> "Mfanyabiashara huyo alikuwa akisumbuliwa na  ugonjwa  ulioathiri mfumo wa koo pamoja na mfumo wa chakula."

Kamanda huyo alisema kwa sasa jeshi la polisi linaendela na uchunguzi ili kubaini ukweli juu ya kifo cha mfanyabiashara huyo ili atua mbalimba za kisheria zeweze kuchuliwa.

Alisema mwili wa marehemu umehifadhi katika hosptali ya rufaa ya KCMC kwaajili ya kuandaa taratibu za mazishi ya mfanyabishara huyo.

No comments:

Post a Comment